Ticker

10/recent/ticker-posts

KITUO CHA AFYA MURIET CHAKABILIWA NA TATIZO LA UHABA WA WAFANYAKAZI

Na Woinde Shizza Michuzi  Tv,Arusha

Uhaba wa wafanyakazi katika katika kituo Cha afya Cha muriet kilichopo jijini Arusha Bado ni changamoto  kubwa inayoikabili kituo hicho .

Akizungumzia swala hilo mganga mkuu  wa jiji la Arusha Dr Simon Chacha wakati akisoma historia ya kituo hicho mbele ya  katibu mkuu wa ofisi ya Rais (TAMISEMI)mhandisi Joseph Nyamuhanga amesema kuwa kituo hicho Bado Kina  changamoto ya wafanyakazi  .

Alisema kuwa kituo hicho kina jumla ya wafanyakazi 25 na kuna  uhitaji waambao ni wachache sana na hawatoshi kwani walitakiwa watumishi  52   katika kila  kituo Cha afya .

Chacha ameendelea kusema kuwa katika kituo hicho Bado pia wanauhitaji wa vifaa  vya matibabu ikiwa  baadhi ya vifaa wamevipata kwa kupitia  mfuko wa ndani ya jiji katika mapato pia kwa kuwezeshwa na wawekezaji ikiwa mkuu wa mkoa na wengine.

Alisema kuwa ujenzi wa Kituo hicho kimegarimu kiasi cha shilingi  billion 1 na elfu 59  ambapo halmashauri ilichangia milion 359  na serikali  kuchangia milion 700 ,  huku akibainisha kuwa kituo hicho  kinahudumia mitaa 13  ambayo ina  wakazi wasiopungua  elfu  50  

Aidha alitaja majengo yaliokamilika had I sasa ni pamoja na jengo  ya exray, OPD, maabara, jengo la mama na mtoto  ,upasuaji pamoja na jengo la kuhifadhia maiti.

Kwa upande wake   katibu mkuu wa ofisi ya Rais TAMISEMI mhandisi  Joseph Nyamuhanga alifurahishwa na Kazi iliofanywa alishukuru  halmashauri kwa kununua vifaa vya utendaji kazi katika kituo hicho pia alisema kuwa wao kama serikali watahakikisha wanapata vifaa  pamoja na kuleta watumishi ili waweze kufikia idadi inayotakiwa ili waweze kutoa matibabu mazuri kwa wananchi .

"Tatizo Hilo la uhaba wa wafanyakazi kazi Bado lipo kwenye  vituo afya ,zahanati na hospital   sisi kama serikali tutajitahidi kukamilisha idadi ya watumishi hao inaongezeka napenda kumaliza kwa kuwashukuru wafanyakazi wa kituo hichi   kwa kuendelea kufanya kazi kwa umahiri na kuhakikisha wagonjwa wanavutiwa na huduma yenu " alisema Nyamuhanga

Akizungumza meya wa jiji  kalist Lazaro amesema kuwa anamshukuru Sana katibu mkuu kwa kutembelea kituo hicho ba kuendelea kusema  halimashauri yao itakapokuwa na uwezo hawatasubiri kufanya maendeleo  ili kuwasaidia wananchi wake.

"Tunahitaji kufanya maendeleo Kama halmashauri ili kuipunguzia serikali mzigo napenda kusema Mimi na  mkurugenzi wa jiji tunaendelea kushughulikia miradi ili kuinua maendeleo katika mkoa wetu " Lazaro.
 Picha ikionesha Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI mhandisi  Joseph Nyamuhanga akizungumza na Wanahabari wakati wa ziara


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2ZYwZwn
via

Post a Comment

0 Comments