Ticker

10/recent/ticker-posts

Mose Iyobo Adaiwa Kusepa WCB Mwenyewe Afunguka A-Z

Mose Iyobo Adaiwa Kusepa WCB Mwenyewe Afunguka A-Z
DANSA maarufu Bongo kutoka kundi la Wasafi , Moses Iyobo amefafanua uvumi wa kutaka kuondoka kwenye kundi hilo na kujitenga. Akizungumza na Spoti Xtra, Iyobo amesema hayo maneno hata yeye ameyasikia lakini hayana ukweli wowote na yote yamezuka kwasababu ya kutoonekana katika video ya Tetema ya Diamond na Rayvanny.

Anasema hakuonekana kwa sababu ratiba ziliingiliana kwani siku waliyokuwa wanashuti yeye kuna kazi zake alikuwa anafanya.



“Kwanini niondoke WCB? Yaani kutokuwepo kwenye video ya Tetema tu basi ishakuwa nongwa? Mimi ni WCB damu yaani sio wa kuondoka leo wala kesho na sijawahi kuwaza.



“Sababu ya mimi kutowepo kwenye video ni kutokana na ratiba ambazo ziliingiliana ndio maana sikuwepo lakini sio kwamba najitenga ama nataka kujitoa hapana kwakweli hizo habari ni za uongo,” alisema Mose.

from UDAKU SPECIAL BLOG https://ift.tt/2TgECdE
via

Post a Comment

0 Comments