Ticker

10/recent/ticker-posts

LAAANA:Shuhudia hapa Baba Alivyonaswa Gest na Mwanaye wa Kumzaa

KIMENUKA! Fadhil Mshamu, mkazi wa Kibaha mkoani hapa anakula Krismasi na Mwaka Mpya wa 2018, akiwa na stresi kufuatia kusomewa shitaka la kumdhalilisha binti yake wa kumzaa jina linahidhiwa kwa sababu za kimaadili.

Kesi hiyo ilitajwa wiki iliyopita ambapo itaanza rasmi kusikilizwa mapema Mwezi Januari, mwakani katika Mahakama ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani.



Mshamu alikutwa na kasheshe hilo baada ya miezi kadhaa kunaswa akiwa na binti yake wa kumzaa kwenye nyumba moja ya kulala wageni (gesti) huko Kibaha huku kukiwa na madai ya kumtaka kingono.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Mshamu alinaswa akiwa na binti yake huyo baada ya kuwekewa mtego kufuatia taarifa za kumsumbua kwa muda mrefu akidaiwa kumtaka kimapenzi.

Kwa mujibu wa chanzo chetu kutoka ndani ya familia ya Mshamu, baada ya kunaswa kwenye mtego huo uliowashirikisha polisi na ndugu wa familia hiyo, Juni 26, mwaka huu, Jeshi la Polisi lilimfungulia Mshamu jalada la uchunguzi ambalo lilipelekwa kwa Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali (DPP) ambapo naye baada ya kuiona kesi hiyo, aliamuru ipelekwe mahakamani.

Ndugu huyo wa familia alilieleza gazeti hili kuwa, kufuatia sakata hilo, wiki iliyopita Mshamu alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa shitaka la kutaka kumdhalilisha binti yake huyo ambaye ni mwanaye wa kumzaa kisha kutajwa tarehe ya kuanza kusikilizwa.

Kesi hiyo inatarajiwa kusikilizwa mahakamani hapo Januari 2, mwakani ambapo waandishi wetu wataendelea kufuatilia sakata hilo mahakamani hapo na kukuletea habari kamili.



AMA kweli mastaa hawaishiwi vimbwanga! Hayo yalidhihirika usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita baada ya staa wa kike wa Bongo Fleva, Esterlina Sanga ‘Linah’ kudaiwa kutelekeza mwanaye mchanga na kunaswa akibanjuka na jamaa ambaye ni meneja wa wasanii wa Bongo Fleva, Petit Man.

Tukio hilo lililonaswa na Ijumaa Wikienda lilijiri ndani