Ticker

10/recent/ticker-posts

Njia za kujenga uwezo wa kujiamini

Image result for chumvini imageNi vigumu kuelezea moja kwa moja kujiamini maana yake nini? Lakini mtazamo wa mwanadamu juu ya namna wenzake wanavyomchukulia inaweza kuwa kutafsiri ya neno kujiamini. Ikiwa utajilinganisha na wengine na hatimaye kuhisi aibu, ujue unakabiliwa na tatizo la kujiamini.

Kimsingi kuna mambo mengi yanayoweza kumfanya mtu asijiamini mbele ya wenzake, kiasi cha kujiona duni kwa hili na lile na wakati mwingine hali hiyo humfanya ashinde kufanya hata mambo ambayo anayajua na kwamba amekuwa akiyafanya kila siku

Kisaikolojia huu ni ugonjwa ambao unaweza kuathiri uwezo wa mtu kibaiolojia, nikimaanisha kwamba mtu anaweza kuwa si mlemavu wa miguu, lakini akatembea mbele za watu upande upande, anaweza kuwa na akili lakini akajikuta hawezi kuzitumia kwa sababu si mwenye kujiamini.

Kama ilivyo kwa magonjwa mengine, kuponywa kwa tiba, tatizo hili la kutokujiamini nalo linatakiwa litibiwa. Zipo njia nyingi ambazo mtu anaweza kuzitumia kujenga hali ya kujiamini, Kwangu mimi yako mambo 10 ya msingi ambayo mtu akiyazingatia na kuyafanyia kazi anaweza kuondokana na hali ya kutokujiamini.

Kuchagua mavazi

Ingawa mavazi hayatafsiri moja kwa moja hali ya mtu, lakini katika lugha ya mawasiliano yasiyokuwa na sauti uvaaji wa mtu ni utambulisho wake. Hivyo kama mtu hazingatii uvaaji unaokubalika katika jamii anakuwa katika wakati mgumu wa kujiamini, hasa kama akilini mwaka yeye mweyewe atatambua kuwa amevaa vibaya.

Hii ina maana kwamba kama mtu anataka kujenga hali ya kujiamini, lazima achague mavazi yanayoendana na mazingira na yawe ni mavazi ambayo mwenyewe akiyafikiria yahatamfanya ajione ni wa tofauti kwa wenzake. Mavazi hujenga muonekano, ukionekana vizuri mbele za watu utajiamini, hivyo kuwa makini na uchaguzi wa mishono ya nguo unazovaa kila siku.

Kutembea haraka

Njia rahisi ambayo imethibitika kuweza kumuondolea mtu hali ya kutokujiamini ni kutembea kwa mwendo wa haraka. Haipendezi unapokuwa njiani kutembea kama mgonjwa, uliyechoka. Ukiwa hivyo ni rahisi sana kuwafanya watu wakukodolee macho ambayo yatakufanya wewe uhisi tofauti. Utemebeaji wa haraka una faida nyingi, lakini kubwa kabisa ni kuwafanya watu wengine wakuone wewe ni mtu wa kazi usiyetaka kupoteza muda wako, mtu makini na mwenye mipamgo. Kitaalamu mwendo unaoruhusiwa ni wa asilimia 25, usizidi sana kiasi cha kuonekana kama unakimbia.

Muonekano sahihi

Namna mtu mwenyewe anavyouweka mwili wake linaweza kuwa ni tatizo la kumfanya ashindwe kujiamni. Kwa mfano,mtu kama si mlemavu lakini akajikuta anatembea miguu upande, mabega juu, kichwa chini au juu sana au kutembea akiwa anadundika kama mpira, ni vibaya kwa vile kitalaamu huchangia kumuondolea mtu ujasiri mbele za watu.

Ushauri wangu ni kwamba mtu anatakiwa kuupa mwili wake umuhimu na kuuweka kama alivyoumbwa, haifai kuwa mtu wa kuinama na kuficha uso, kusimama tenge pale unapoitwa au kuwa mbele za watu. Si vema pia kung�ata kucha, kujipapasa mwilini au kutazama pembeni. Ni vizuri kila mtu kulinda muonekano wake wa asili mbele za wenzake.

Kujizoeza kujiamini

Njia moja muhimu sana kisaikolojia ya kujenga hali ya kujiamini ni kupenda kusikiliza maneno ya kutia moyo nay a ujasiri kutoka kwa watu maarufu. Kwa mfano, viongozi wenye msimamo, watetezi wa haki za binadamu, wanasiasa wanaotetea maslahi ya nchi bila hofu na kadhalika. Hotuba na maneno yao yakipata sehemu kubwa katika akili ya mtu, lazima yatajenga hali ya kujiamini kama wale anaowasikiliza.

Kukubali matokeo

Ifahamike kuwa ukiwaza kwa kina sana juu ya mahitaji yako, zao litakalofuata hapo ni akili kukuletea sababu za kishindwa kufanikisha mambo unayoyataka. Sababu hizo ukizipa nguvu sana ya kuziwaza zitakupa jibu la haiwezekani. Unapokuwa na mawazo yenye mlango huo wa kutokufanikiwa, uwezo wako wa kujiamini hushuka na kujikuta unashindwa katika mambo uyafanyayo. Katika maisha lazima mtu akawa na wakati wa kuachia mawazo yake na kukubaliana na matokeo yaliyopo hasa pale hali ya kushindwa inapokuwa kubwa.

Kupingana na wengine

Mtu akijiona duni mwenyewe ni rahisi kwake kudhani kuwa watu wengine ndiyo wenye mambo ya kweli na hivyo kujikuta akifuata mkumbo na kupotoshwa katika ukweli. Ili mtu aweze kuwa sahihi katika mawazo ya vile ananvyoamini ni lazima awe na tabia ya kupingana na wenzake. Ni jambo baya kukubaliana na watu katika mawazo yao bila kupinga katika kile unachoamini, kufanya hivyo kunaweza kuyafanya maneno ya uongo ya wengine yakaaminika na kuuacha ukweli wa mtu asiyejiamini ukipuuzwa kwa sababu tu hakuwa na ujasiri wa kukabiliana na hoja za wenzake.

Pendelea kukaa mbele

Katika kujenga hali ya kujiamini ni vizuri zaidi unapokuwa shule, ofisini, kwenye mikutano, semina ukawa na tabia ya kuketi nafasi za mbele. Ni ukweli kuwa, watu wengi hawapendi kukaa sehemu za mbele kwa sababu ya hofu ya kuonekana kwa urahisi na pengine kuwa wa kwanza kuulizwa au kuchangia hoja, tabia hiyo huondoa hali ya mtu kujiamini. Ili kujenga ujasiri ni vema mtu akapendelea kuketi vitu vya mbele na mara nyingi kuwa wa kwanza katika kufanya mambo.

Zungumza bila aibu

Ukimya wa kupita kiasi nao ni tatizo, hasa pale linapokuja suala la kuogopa kuzungumza mbele za watu kwa hofu ya kuonekana hujui. Wapo wanafunzi na wasomo wengi wanapokutana katika vikundi vya mazungumzo maarufu kama Groups Discusions huwa hawapendi kuzungumza wakilenga kujificha na aibu itokanayo na udhaifu wao katika uelewa. Hata hivyo kutochangia mazungumzo na wengine hakuna faida zaidi ya hasara kwa mtu kutoweza kujiamini. Inashauriwa kwamba ili mtu aweze kujenga hali ya kujiamini ni vema akajenga mazoea ya kuongea mbele za watu bila aibu.

Kujenga afya

Kipengele cha kulinda afya ni muhimu sana kwa mtu anayetaka kujenga hali ya kujiamini. Kukonda au kunenepa sana umbo kunaweza kumfanya mtu akajiona wa tofauti na hivyo kupoteza hali ya kujiamini. Hivyo basi kama unakonda hakikisha kuwa unakula vyakula vyenye vitamini ili kuufanya mwili wako usiwe kituko kwa wengine, hali kadhalika kama unanenepa sana fanya mazoezi ili kuupunguza mwili wako. Tafuta afya ili uwe na nguvu za kufanya mambo kwa umakini.

Msaada kwa wengine

Baada ya kufanikiwa katika hatua zote ambazo tumeziangalia hapo juu, jambo jingine la muhimu katika kuhitimisha uwezo wa mtu kujiamini ni kupata msaada wa mawazo kutoka wa watu wengine ambao ni makini katika maisha yao. Kama kuna jambo ambalo linakuwa gumu katika mawazo yako na limekosa ufumbuzi kiasi cha kukufanya usijiamini, washirikishe wengine wakusaidie na kukutia moyo wa kuendelea kukabiliana na hali yakutojiamini.



Miongoni mwa matatizo makubwa kabisa yanayowakabili wanaume katika suala la kujamiiana ni kufika kileleni mapema. Takwimu zisizo rasmi zinaonesha kuwa, wanaume saba kati ya kumi wanakasoro hii.

Malalamiko yanayotolewa na baadhi yao yanakariri kwamba, muda wa kumaliza tendo huwa kati ya nusu dakika na dakika tatu kwa tendo la kwanza, huku wengine wakimaliza hamu katika hatua za awali tu za hamasa ya kimahaba.

Hata hivyo kumetolewa maelezo na nafuu ya ongezeko la muda katika tendo la pili na kuendelea, ingawa bado suala la kutangulia kufika kileleni kabla ya mwanamke limekuwa likiwahuzunisha wanaume walio wengi.

Ndoa na wapenzi wengi wameachana kwa kasoro hii waliyonayo wanaume. Karibu kila kona kunasikika vilio toka kwa wanaume wakilalamika kukabiliwa na tatizo la ufikaji kileleni mapema, ambalo limewafanya waonekane si �keki� kwa wapenzi wao.

Ni ukweli usio pingika kuwa mwanaume anapowahi kufika kileleni kabla ya mwenzake humsababishia kero mwanamke anayeshiriki naye tendo, kwani humwacha njia panda pasipokuwa na hitimisho la raha ya kujamiiana.

Hali hii inatokana na maumbile ya mwanaume yanayomlazimisha kusinyaa uume mara baada ya kuhitimisha mbio zake, ingawa kwa mwanamke kuwahi si tatizo, kwani hakumfanyi ashindwe kumsindikiza mwenzake hadi kileleni.

Pengine utofauti huu ndiyo unaowafanya wanaume wahuzunike zaidi wanapokabiliwa na janga hilo kiasi cha kufikia hatua ya kwenda kwa waganga kutafuta tiba ya miti shamba ili iwasaidie kuepuka balaa ya kutoka uwanjani na aibu.

Ingawa kumekuwa na mafanikio katika tiba asili, lakini bado wanaume wameshindwa kupata ukombozi wa kudumu wa tatizo hili. Wengi wamejikuta wakijiongezea mzigo wa fikra kwa kuzitumaini zaidi dawa, jambo ambalo huwalazimisha kuzitumia kila wanapofanya tendo na ikitokea hawakuzipata, aibu hubaki pale pale.

Kwa kufahamu mikinzamo iliyopo kati ya akili na tiba ya nguvu za kiume na madhara yachipukayo imebainika kuwa, mtu anaweza kujitibu tatizo hilo kwa kutumia kanuni za kisaikolojia, badala ya dawa na mafaniko yasiyo na madhara yakapatikana.

Kimsingi kanuni ya ufanyaji mapenzi iko zaidi kwenye ubongo kuliko mwilini. Kinachotokea hadi mtu akapata msisimko wa kufanya mapenzi si mwitikio wa mwili, bali ni utambuzi wa akili juu ya kiwango cha mwanamke anayefaa kimapenzi.

Inaelezwa kuwa, akili ikishiba vigezo na kutuma taarifa zenye usahihi kwenye mwili viungo hupokea hisia na kuanza kusumbua. Kwa msingi huo kama tunataka kufika kileleni mapema au kuchelewa lazima tucheze zaidi na akili kuliko mwili.

Katika hali ya kawaida nguvu ya kupenda inayomwingia mtu huwa kubwa, lakini suala la kupunguza ukubwa wa hisia lazima lipewe kipaumbele. Jambo kubwa linalowasumbua wanaume wengi wenye tatizo la kufika kileleni mapema ni kuwa na PUPA ya kufanya ngono.

Wengi wao hupokea hisia zilizokuzwa na kwenda nazo katika ufanyaji wa tendo la ndoa. Wataalam wa saikolojia wanasema ili mwanaume achelewe kumaliza, lazima apunguze mhemko unaotokana na kuona, kuhisi na kupagawishwa na staili au chombezo toka kwa mwanamke.

Anachotakiwa kufanya ni kutumia zaidi ya dakika 20 kufanya maadalizi na mpenzi wake kabla ya kuanza tendo. Hii itasaidia kuufanya mhemko wake ushuke na kumuongezea muda wa kumaliza.

Aidha mbinu ya kuidanganya akili lazima itumike ili kuzima taarifa za juu za uzuri wa mwanamke, maumbile na raha ya starehe isipokelewe kwa nguvu kubwa mwilini. Hii ikiwa na maana kuwa kuna kipindi inabidi fikra za mwanume zisihamasike sana kwenye tendo badala yake iletwe mawazoni hali ya kawaida, si ile ya kuweweseka na kuhema hema hovyo. Yafuatayo ni maelekezo ya msingi ya kufanya, ili mtu asifike kileleni mapema:

Mume na mke wanapoingia katika uwanja wa mapenzi wakae kwanza kwa muda, huku wakiwa wamejiachia na mavazi mepesi. Pili wacheze michezo mingi kwa muda mrefu bila kuanza kazi yao. Wakiwa kwenye hamasa hizo wasiwe kimya bali wazungumze na kuulizana maswali ya kimahaba.

Baada ya hapo mbinu nyingine ya kuzuia mbegu za kiume zisitoke ni ile ya kujibana. Inashauriwa kuwa mwanaume akiona dalili za awali za kumaliza bila kujali ametumia muda gani anachotakiwa kufanya ni kukaza misuli ya miguu na kuzuia mbegu kwa mtindo atumiao kuzuia haja ndogo isitoke.

Kujibana huko kunatakiwa kuende sambamba na kuacha kucheza �shoo�. Pacha na hilo mwanaume anatakiwa kuidanganya akili kwa kuilazimisha iwaze jambo jingine hasa la kuhuzunisha ili kuharibu taarifa za raha zilizotumwa mwilini zisiendelee kufanyiwa kazi na hatimaye kumaliza tendo haraka.

Zoezi hili linaweza kuwa gumu katika hatua za kwanza kutokana na kukosea muda sahihi wa kujizuia, lakini mhusika akiendelea kujizoeza atajikuta anaweza na kupata uwezo wa kufanya mapenzi hata kwa saa nzima, hivyo kuondokana na tatizo hilo bila tiba wala madhara.