Ticker

10/recent/ticker-posts

Mwanamuziki Maarufu wa Bongo fleva Adaiwa Kumzalisha Binti na Kumtelekeza Mtoto..Stori Nzima Ipo Hapa

Msanii wa bongo Fleva anayetamba sasa kwa kibao chake cha siwezi,Baraka da Prince amepata kashfa ya kumzalisha binti wa miaka wa 19 aishie Iringa aliyejitambulisha kwa jina la Candy kisha kumtelekeza  mtoto huyo.

Akiongea na redio moja binti huyo amedai mtoto wake na Baraka da Prince ana mwezi mmoja na nusu ambapo alimzaa kwa kwa opresheni mwezi wa Desemba mwaka Jana.baraka

Binti huyo amedai kuwa alianza mahusiano na baraka da Prince wakati alipoenda Iringa kipindi baba yake anafanya kazi huko na badaaye wakakubaliana aje Dar ambapo wakawa wanaishi wote mpaka binti alipopata ujauzito na kurudi Iringa kwenda kulea ujauzito huo.

Candy akaendelea kusema kuwa baada ya yeye kurudi Iringa hakupata matunzo yoyote kutoka Baraka da Prince hata alipojifungua.Binti anasema kila akijaribu kumtafuta Baraka kwenye simu hudai yuko bize na mara nyingine humtolea maneno ya kuudhi.

Candy amedai kuwa ana ushahidi wa picha kadhaa za Baraka da Prince na mtoto na juzi tu Baraka alivyoenda kufanya show alienda kuwaona na kutoa ahadi kibao lakini mambo yamebaki vile vile hakuna matunzo yoyote.