Ticker

10/recent/ticker-posts

ROSE NDAUKA AJIBU TETESI ZA KUWA NA UHUSIANO NA SHETTA


Baada ya kuenea tetesi kuwa mke wa Shetta ‘Neila Yusuf’ anadai talaka kwa mume wake kutokana na Rose Ndauka kuingilia ndoa yao, Ndauka amevunja ukimya.
11208267_1018831591463131_2026634416_n
Akiongea kwenye kipindi cha Mkasi, Ndauka alikanusha kuwahi kuwa na uhusiano na rapper huyo.
“Kuna siku nilikuwa kwa Diamond, Mama Kayla alikuwepo, kwahiyo akawa amenifuata kunisalimia, Dareen akawa ananiambia umemuona ‘mama Kayla?’ Nikamwambia yupo wapi? akaniambia ndio huyu hapa! Nikawa nacheka nikamwambia ‘mambo’, nikamwambia nasikia umeondoka kwako kwaajili yangu? Akaanza kucheka, akaniambia ‘sio kweli mbona hakuna kitu kama hicho.’ Kwahiyo nikacheka kwa sababu mtu mwingine anaweza kucreate tu kitu kwa sababu tu hawajamuona Rose kwenye magazeti. So wanataka kumweka kwenye zile skendo ili awe mmoja kati ya wasanii wenye skendo,” alisema Ndauka.

-bongo5