Stori: Gladness Mallya na Mayasa Mariwata WAKATI mastaa kadhaa wa
kike wa filamu Tanzania wakionekana umri wao kuwatupa mkono, lakini
wakiwa hawana ndoa wala watoto, baadhi yao wamefunguka kuwa wanahitaji
zaidi kupata uzao kuliko kuishi maisha ya kuolewa.
Staa wa filamu wa filamuBongo, Anti Lulu akipozi. Wakizungumza kwa
nyakati tofauti jijini Dar es Salaam, walisema suala la ndoa ni
majaaliwa na si jambo unaloweza kupanga, kwa vile mwenye uwezo wa
kufanya hayo yote ni Mungu, kama ilivyo katika kuamua kuzaa au la.
Coletha Raymond ‘Koletha’, alisema katika maisha ya Kitanzania,
wanaume ndiyo wenye uwezo wa kuamua. wataoa lini na ikawa kwa sababu wao
ndiyo wanaotongoza, lakini mwanamke hawezi kusema.
“Kuolewa natamani sana lakini bado sijapata mwanaume sahihi,
naendelea kumuomba Mungu anipe, nawaomba na wengine wanisaidie kuomba,
kuhusu kuzaa niko tayari hata kama sijaolewa,” alisema.
Staa wa filamu wa filamuBongo, Baby Madaha. Kauli kama hiyo ilitolewa
pia na msanii wa filamu Lulu Semagongo ‘Anti Lulu’ aliyesema yupo
tayari kuzaa hata kabla ya ndoa kwa sababu kuitwa mama kwake ni muhimu
kuliko ndoa.
Lakini katika hatua ya kushangaza, Baby Madaha ambaye pia anafanya
muziki, alisema hana anachotamani kati ya ndoa wala mtoto, isipokuwa
kitu muhimu kwake kwa sasa ni pesa.
Staa wa filamu wa filamuBongo,Salma Jabu ‘Nisha’. “Katika maisha
yangu sina mpango wa kuolewa wala kuzaa, ninachotafuta zaidi ni pesa na
umaarufu, dunia nzima initambue, sijali cha umri wala nini, hayo ndiyo
maamuzi ya maisha yangu.”
“Mimi siwezi kujua nitaolewa lini kwa sababu Mungu ndiye anajua ubavu
wangu uko wapi na anakuja kwangu lini, pia siwezi kuwa na uhakika kama
niliyenaye ndiyo ubavu wangu.“Naweza nikasema naolewa mwaka huu kumbe
nikaja kuolewa miaka miwili mbele. Suala la kuzaa kiukweli hakuna kitu
natamani sasa hivi kama mtoto, hili sizungumzii sana, litakuwa ni
sapraizi kwa mashabiki zangu,” alisema Tamrina Poshi.
Staa wa filamu wa filamuBongo, Coletha Raymond ‘Koletha’ akipozi. Kwa
upande wake, Salma Jabu ‘Nisha’ alisema ndoa ni heshima kwa mwanamke,
lakini anachoamini jambo jema hupangwa na Mungu.
“Mungu anatengeneza tutakayerandana na kupendana kiukweli na kuja
kudumu kama wazee wetu walivyokuwa, akimleta hata leo nitaolewa,”
alisema.