Bishoo, Quick Rocka amekanusha kuwa na Uhusiano wa kimapenzi na muigizaji wa filamu, Kajala Masanja
Akizungumza na 255 ya XXL, Clouds FM, Quick amesema ana girlfriend hivyo uvumi huo unaweza ukamharibia uhusiano wake.
“Nasema hapana Kajala mimi sister yangu, tunafanya naye kazi na nimeunganishwa na Lamata.
Lamata
ni director ninayemmfahamu zamani kidogo kipindi kile tunafanya ‘Mbwa
Mwitu’ tulikuwa wote, Lamatah, Hemedy! Unajua mnavyofanya movie ni
tofauti na kufanya video, kwa mfano wakati tunafanya ile movie ya
Wolper, tulikaa Magomeni kambini ili kujenga chemistry.
Unajua mnapoigiza kuna vitu lazima viendane. Sisi ni kambi moja inabidi mchongo tuufanikishe,” Alisema Quick Rocka.
“I
have a girlfriend, anavyosikia hivi vitu mimi kwa upande mmoja
inaniharibia na sijui yeye pia ana mtu wake huko kwahiyo tuna wazazi,
tuna watu wetu wa karibu ambao wanatuangalia, watu ambao wametupenda na
wametuamini hivyo halafu wakija kusikia mambo haya kwenye media wataona
kumbe huwa hamfanyi kazi, wao wanachukulia serious. Sio vitu vya kweli.”
UMEICHEKI HII ? True Story: Nampenda Binamu Yangu Sana Hasa Kimapenzi.
-jimmcarter
-jimmcarter