Msanii
wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha akiwa na mwanae.“Mimi ni mama bora,
ndiyo maana nimekuwa nikiulizwa na vyombo mbalimbali vya habari kama
nina mtoto nilikuwa nakataa kwa sababu sitaki kumkuza mwanangu kupitia
media, ni bora akishakua mwenyewe atajitangaza kupitia kazi zake,
sikupenda kumwanika kwenye vyombo vya habari kwa sababu siyo maadili
mema,”alisema Nisha.
MASTAA wana mambo! Baada ya kukataa kwa muda mrefu kwamba hajawahi
kuzaa, msanii wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amemwanika mwanaye
anayejulikana kwa jina la Iptysam Othman ‘Angel’ mwenye umri wa miaka
10.
Salma
Jabu ‘Nisha akiwa kwenye pozi.Hata hivyo alikana kwa nguvu zote madai
kwamba ana watoto wawili, akisisitiza kuwa anaye mmoja tu na hakutaka
kumweka wazi kwa vile aliamini hali ile ingemuathiri kisaikolojia,
ingawa hakufafanua.