Stori: Imelda Mtema
Mastaa wawili hapa Bongo ambao huko
nyuma walikuwa katika bifu kali, Wema Sepetu na Penny Mwingilwa
wameonekana kumkejeli aliyekuwa mpenzi wao, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa
kutumia neno Project.
Mastaa hao walionekana wameweka picha yao wakiwa pamoja wamejilaza chini nyumbani kwa Wema na kuandika kuwa wakiwa katika Project yao neno ambalo lilitumiwa na Diamond akiwa na mwanadada Zarina Hassan ‘Boss lady’ anayedaiwa kutoka kimapenzi na mwanamuziki huyo.
Gazeti hili lilifanikiwa kuzungumza na Penny kwa njia ya simu ambapo alisema kuwa siku hiyo walikutana na kuzungumza na rafiki yake huyo wa muda mrefu na mambo ya project yalitokea tu. “Sisi tulimisiana sana na tulikutana na kuzungumza mambo mengi ya zamani, hiyo project iliingia tu,” alisema Penny. GPL
Mastaa hao walionekana wameweka picha yao wakiwa pamoja wamejilaza chini nyumbani kwa Wema na kuandika kuwa wakiwa katika Project yao neno ambalo lilitumiwa na Diamond akiwa na mwanadada Zarina Hassan ‘Boss lady’ anayedaiwa kutoka kimapenzi na mwanamuziki huyo.
Gazeti hili lilifanikiwa kuzungumza na Penny kwa njia ya simu ambapo alisema kuwa siku hiyo walikutana na kuzungumza na rafiki yake huyo wa muda mrefu na mambo ya project yalitokea tu. “Sisi tulimisiana sana na tulikutana na kuzungumza mambo mengi ya zamani, hiyo project iliingia tu,” alisema Penny. GPL