...Akiendelea kuandaa.Kwa
mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo lilijiri wikiendi iliyopita kwenye
Makaburi ya Ufi yaliyopo maeneo ya Ubungo-Kisiwani jijini Dar, mishale
ya saa nne usiku.Ulozi!
Chipukizi sinema za Kibongo, Fatuma Ayubu ‘Fetty’ amenaswa makaburini
akiwanga katika kile kinachodaiwa kuwa ni kutekeleza masharti ya
‘sangoma’ ili ajipatie umaarufu na kuwafikia mastaa kama Wema Isaac
Sepetu, Jacqueline Wolper Massawe na Elizabeth Michael ‘Lulu’
Awali,
ilidaiwa kwamba, Fetty ambaye anaonekana kwenye Filamu ya House of
Death akiwa na mwigizaji Kulwa Kikumba ’Dude’ alitinga kwenye makaburi
hayo akiwa ameshika kimfuko huku akiangaza huku na huku kisha akatoa nazi na kuivunja huku akinuiza maneno bila kujua kuna mtu alikuwa akimpiga picha.