Ticker

10/recent/ticker-posts

DUUUH!: BABY MADAHA ATILIA SHAKA AFYA YA ‘MKONGO WA WOLPER’..AFUNGUKA MENGI...ANGALIA HAPA

Msanii wa filamu na muziki, Baby Joseph Madaha
Stori: MAYASA MARIWATA
Msanii wa filamu na muziki, Baby Joseph Madaha amesema ana wasiwasi na afya ya mwanaume Mkongo anayefahamika kwa jina la Mwani aliyewahi kuwa mpenzi wa Jacqueline Wolper.

Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Baby Madaha alisema, hofu yake hiyo inatokana na namna mwanaume huyo anavyotapanya pesa huku akitangaza dau kubwa ili kuwapata mastaa wa kike.
Mkongo anayefahamika kwa jina la Mwani aliyewahi kuwa mpenzi wa Jacqueline Wolper.

“Kimsingi mimi nina wasiwasi na afya yake, asije akawa anataka kutumaliza. Mimi simhitaji hata kama ana mamilioni yake. Hofu yangu ni hii tabia yake ya kutaka kutupitia sisi mastaa, wanaokubali kuwa naye eti kisa ana mkwanja nawaonea huruma,” alisema Baby Madaha