Ticker

10/recent/ticker-posts

HATI YA MUUNGANO YAWASILISHWA BUNGENI

Makamu mwenyekiti wa bunge maalum la katiba, Samia Suluhu Hassan amesema amepokea hati ya makubaliano ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliyothibitishwa kisheria.
 
Hati hiyo imefikishwa bungeni hapo baada ya mjumbe wa bunge hilo, Tundu Lissu kuomba hati hiyo ioneshwe hadharani siku mbili zilizopita.
 
Waziri wa nchi ofisi ya rais, Stephen Wasirra alieleza kuwa ametimiza ahadi yake aliyoitoa awali kuwa hati hiyo ingefikishwa bungeni ndani ya siku mbili.
 
Katika hatua nyingine, wajumbe wa bunge hilo maalum la katiba leo wameendelea na majadiliano kuhusu sura ya kwanza na ya sita ya rasimu ya katiba huku suala la muundo wa serikali za muungano likichukua nafasi kubwa.

Post a Comment

0 Comments