HAPATOSHI NDANI YA SERENA HOTEL LEO NOVEMBA 8
MAMA ASHA BILAL NDANI NA MASTAA KIBAO
Na Andrew Chale
"LEO ndio Leo, lile Onesho la Usiku wa
Khanga za Kale 2013, 'Extra Vaa Khanga Party' ndani ya Hoteli ya Serena
jijini Dar es Salaam, leo Ijumaa ya Novemba 8.
Katika onesho hilo, jioni ya leo, Mke
wa wa Makamu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi Asha Bilal
anatarajia kuwa mgeni rasmi katika kusindikiza usiku huo ambao pia
utapambwa na mastaa mbalimbali wa ndani na nje ya nchi, ikiwemo burudani
murua kutoka kwa bendi ya Mashauzi Classic.
Mkurugenzi wa Fabak Fashion, Asia
Idarous, ambao ndio waandaji wa maonyesho hayo, amesema tofauti na
maonyesho mengine yaliyotangulia, Kanga ya Kale ya mwaka huu ina ladha
tofauti kidogo ilikuwapa radha wadau wake..
"Licha ya kuonyesha matoleo mapya na
mitindo ya kanga pia kuonyesha yale ya zamani ili kuleta vionjo zaidi
kwa wavaaji wa sasa, tunakusudia kutoa darasa kuhusiana na thamani ya
kanga japo kwa muda mfupi tu", alisema.
Na kuongeza kuwa, usiku huo vazi la
khanga ndilo litakuwa maalumu kwa wadau watakaohudhuria sambamba na
kupinga matumizi ya dawa za kulevya.
Kiingilio katika onyesho hilo ni sh
30,000 na viti maalumu itakuwa ni sh 50,000 ambako tiketi zinaendelea
kuuzwa Fabak Fashions Mikocheni na Gift Shop Serena Hotel pamoja na
mlangoni hapo hapo Serena hotel.
Aidha, usiku wa Khanga za Kale
umedhaminiwa na Redd's, CXC, Clouds FM, Vayle Spring, Magic FM, Eye
View, Amina Design, Kabile, Voice of America, Origin Unite, Channel Ten,
DTV, Times FM, Michuzi Media Group, Event Light na Miss Tanzania, New
Africatv.com, Kajuna blog,Vijimambo blog na wengineo kibao.
Maonyesho ya Kanga za kale nchini yanafanyika kwa mara ya tano tangu pale yalipoanzishwa rasmi mwake mwaka 2008
Mwisho
0 Comments