Ticker

10/recent/ticker-posts

Mrembo Tessy Chocolate Afungukia Tetesi za Aslay Kutomuhudumia Mtoto Wao


Mzazi mwenzake na Staa wa Bongo fleva Aslay Isihaka, Tessy Chocolate amefungukia tetesi zinazodai kuwa baba wa Mtoto wake huyo amegoma kumuhudumia mtoto wao baada ya wao kuachana.

Kumekuwa kuna tetesi kwenye mitandao ya kijamii kuwa tangu walipoachana miezi michache iliyopita Aslay amemsahau kabisa binti yake Moza na kuwa busy na wanawake wengine kiasi ya kwamba hakumbuki hata kutoa pesa ya matumizi.



Lakini Mama Watoto Wake anayejulikana Kama Tessy Chocolate amekana tetesi hizo na kusema Askay ni baba mzuri sana kwa binti yao na anashukuru amekuwa akimuhudumia Mtoto wao.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo, Tessy Chocolate alifunguka haya kuhusu uhusiano Wake na Baba Watoto Wake huyo:


Hizo stori hazina ukweli wowote kusema ukweli mimi nashukuru kuwa Aslay anatimiza majukumu yake kama baba anavyotakiwa na kama unamfatilia utaona anamposti sana mtandaoni angekuwa amuhudumii nisingeweza kumruhusu amposti lakini namshukuru kila siku kwa kuwa baba bora kwa binti yake”.


Lakini pia Tessy Chocolate ameweka wazi kuwa hana Bifu na Baba Mtoto Wake hivyo hata akiwa na wapenzi wengine yeye hana neno kwa sababu kila mtu ana maisha yake kwa sasa.Aslay