Ticker

10/recent/ticker-posts

Baby Madaha Ajikosha, Ampa Tano Makonda..!!!

MWANAMUZIKI Baby Joseph Madaha amefungukia uamuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda wa kuanza kudili na wauzaji na watumiaji wa madawa ya kulevya akisema kuwa, huenda ikasaidia mastaa wengi kubadilika. Akipiga stori na Ijumaa

hivi karibuni, Baby Madaha ambaye naye aliwahi kukwaa skendo ya kudaiwa kusafi risha unga kwenda Uarabuni, alisema kuwa anajua kweli mastaa wengi ni watumiaji na wasafi sharisha wa unga hivyo kitendo cha baadhi yao kutaitiwa, kinaweza kuwa mwanzo mzuri.

“Niliwahi kudaiwa kusafi risha unga lakini haikuwa kweli. Wanaouza na kutumia wanajulikana, hivyo mimi nimpe tu tano Makonda kwa hatua hii nzuri, naamini huko tuendako jitihada hizi zitazaa matunda,” alisema Madaha