Ticker

10/recent/ticker-posts

POLISI WA KIKE WA KIISLAMU WARUHUSIWA KUVAA HIJABU



Serikali ya Scotland imeidhinisha vazi la hijabu na kulijumuisha kwenye sare za maafisa wa polisi wa kike wa Kiislamu ili kuongeza idadi yao katika idara hiyo.
Mkuu wa idara ya polisi nchini humo Phil Gormley, ametoa maelezo na kubainisha furaha kubwa kwa kutangaza uamuzi huo, na kufahamisha nia yao kutaka kusaidiana na maafisa wa Kiislamu katika suala la usalama wa taifa.
Muungano wa maafisa wa polisi wa Kiislamu SPMA nchini humo pia ulitoa maelezo na kufahamisha kwamba uamuzi huo utaweza kuimarisha mahusiano bora kati ya jamii za Scotland na jumuiya ya Kiislamu.
Mkuu wa SPMA Fahad Bashir alisema, ''Uamuzi huo uliochukuliwa na serikali ni sahihi. Tunapata faraja kuona nchi yetu ikichukuwa hatua muhimu kama hizi zenye mwelekeo mzuri.''
Hapo awali, maafisa waliokuwa wakiruhusiwa kuvaa hijabu walikuwa ni wale waliohudumu kwa miaka zaidi ya 15 na wanaoshikilia nyadhifa za juu.
Katika mwaka 2001, sare rasmi za polisi zilitambulishwa ambapo hijabu pia ilijumuishwa.