Ticker

10/recent/ticker-posts

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA NAYE AMEANZA KAZI RASMI ......JANA KAANZA NA HAYA BAADA YA KUTUA GEITA.




"Hatukatai kuwa na wawekezaji wachimbe lakini uchimbaji uwe na faida kote wao wapate na wananchi wapate kwa hiyo hatunabudi kusimamia vizuri na kuhakika kwamba wananchi wa Geita wanafaidika na rasilamali ambayo Mwenyezi Mungu amewapangia."
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa Geita Mhe. Fatma Mwassa wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa GGM Mkoani Geita jana Januari 04,2016 kwa ajili ya kuanza ziara ya siku mbili ya kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo Mkoani humo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na baadhi ya wawekezaji wa Mgodi wa GGM Mkoani Geita alipowasili Uwanja wa ndege wa GGM Geita jana Januari 04, 2016 kwa ajili ya kuanza ziara ya siku mbili ya kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo Mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa Geita Mhe. Fatma Mwassa akizungumza wakati akitoa Taarifa ya Maendeleo ya Mkoa wa Geita, kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia), katika kikao kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, jana Januari 4, 2016. Katikati ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Injiani Gerson Lwenge.
www.masamablog.com