Zinedine
Zidane alimsifia Gareth Bale kwamba ni mchezaji wa tofauti sana, baada
ya summer kufika mwaka 2013 akahamia Real Madrid. Sasa wasiwasi umetanda
kwa Hazard kuwa na uwezekano wa kuhamia Real baada ya Zidane kumsifia
hivyo hivyo Hazard akimfananisha kama Cristiano na Messi kwa sasa.
Jose
Mourinho akijibu kuhusu maneno ya Zidane alisema kwamba kama Real
inamtaka Hazard, yeye (Mourinho) angekua wa kwanza kujua.Lakini kama ni
kweli wanamtaka nay eye hajui basi itawagharimu £100 million kwa kila
mguu wa Hazard.
Mourinho
ambae leo ana mechi na Arsenal alisema kwamba haamini kama Real
wanajaribu kum-sign Hazard kwasababu bado hawajamwambia. Uhusiano wake
na rais wa timu na CEO hautoi nafasi ya kitu kama hicho kutoka nyumba ya
mgongo wake. Lazima wangemwambia kwasababu wana aminiana kikamilifu.
Chochote kinaweza kutokea na Real Madrid kwenye kuweka mzigo mzito kumpata yule wamtakae, sio tatizo kubwa kwao. Tusubili tuone.
0 Comments