Nimesikitishwa Sana na habari
zilizoandikwa na moja ya chombo cha habari, kuwa eti nliwanyanyasa
wasanii wenzangu Nyota ndogo na Susumila, kwa kuwafukuza kwenye VIP
lounge na sijui eti niliwazuia wasitumie maji ya chupa hivi inaingia
akilini kweli hii!!!?? Ningependa kutumia nafasi hii kuwajulisha
mashabiki zangu waliokutana na story hizo kuwa sio za kweli ni zenye
lengo la kudhoofisha Mahusiano yetu mazuri ya wasanii Wa Africa
mashariki..kama BigEye ya Uganda ilivyowahi kuandika habari za
upotoshaji Kati yangu na Jose Chameleone..
Pia Nawasihi @Bongofive ni vyema
mtambue Nafasi yenu kwenye jamii kwa sasa, Kuweni makini na baadhi ya
habari mnazo post ama kureport kutoka baadhi ya mitandao, zinavunja
mahusiano mazuri ya wasanii wa East Africa...kumbukeni kuna watu wana
tabia ya kujudge kitu kwa kusoma kichwa cha habari tu pasipo kufuatilia
undani wa habari...Yawezakuwa mwaandika kwa nia njema tu, lakini ni
vyema muwe mnapata na uhakika kwanza kabla ya kuripoti, hususan story za
kutengeneza chuki kama hizi....kufanya hivyo ndiyo mtasaidia kukuza
industry yetu ya East Africa...