Msanii maarufu wa filamu nchini King Majuto amesema kuwa ana nia ya kufanya filamu ya pamoja na Wema Sepetu na Diamond Platnumz.
Akizungumza
na Bongo5, King Majuto ambaye filamu zake nyingi zinafanya vizuri
sokoni alisema kuwa amekutana na Wema hivi majuzi na kumueleza hilo na
kumtaka azungumze kuhusu project hiyo ili Diamond akikubali wafanye kazi
pamoja.
Majuto
alisema kuwa sio kwamba yeye ameshindwa kuzungumza na Diamond bali
kwasababu ameanza kukutana na Wema ndiyo akamweleza kwanza.
“Hivi
karibuni nilikuwa na Wema, nimemwamia aongee na Diamond ili tufanye
filamu ya pamoja mimi Wema na Diamond, hata Diamond ninawe kuzungumza
nae sema nimeanza na Wema Kwanza, akikubali mtasikia tu” alisema King Majuto ambapo pia alisema ili kucheza filamu ya mtu ni lazima alipwe mil.3 cash.
Ingawa
uwezo wa Diamond katika filamu bado haujulikani lakini kama mastaa hao
wote watu wakiwa ndani ya filamu moja na kupata msambazaji mzuri na
mkweli ni lazima wafaidike kwa mauzo makubwa ya filamu hiyo.
0 Comments