Drake amekuwa moja ya mastaa ambao wamekuwa wakikaa kwenye headlines mara kwa mara kutokana na sababu mbali mbali.
Safari
hii Drake ameangusha kitita kikubwa cha fedha wakati akiwa anaharakisha
kuingia ndani ya club ambapo waliomuona wanasema jamaa alikuwa kama
amekasirishwa na kitu hivi, kwa hiyo hata huko alikokuwa anaingia huenda
hakukuwa na jambo la kheri.
Staa
huyo alikuwa anasherehekea birthday yake wikiendi iliyopita Club
Stadium, Washington D.C Marekani ambapo baadhi ya watu waliokuwa ndani
ya club wanasema huenda Drake alikasirishwa na kitendo cha mmoja ya
marafiki zake kupigwa na mtu asiyefahamika.
Moja
ya sababu ambazo huwa zinamuweka Drake kwenye headlines ni ugomvi, kwa
hiyo kama aliingia kushiriki ugomvi wowote ndani ya club, bado si tukio
geni kwa wale wanaomfahamu staa huyo.
Credit:Millardayo