Ticker

10/recent/ticker-posts

SIMULIZI: Hakika Yalionikuta Maishani Ni Mengi - Sehemu ya kwanza (01)

 

Uhamisho wangu wa kikazi kwenda

Tanga

ulikuja kama adhabu kutokana na

ukiukaji wangu wa maadili ya jeshi la polisi

nikiwa

muajiriwa wa jeshi hilo.

Nilijiunga na jeshi la polisi miaka mitano

iliyopita mara tu baada ya kuhitimu

kidato

cha sita huko Kagera ninakotoka.

Nilipomaliza mafunzo yangu ya upolisi

huko Moshi nilipangiwa kuanza kazi jijini

Dar. Mimi na wenzangu kumi na wanane

tuliuopangiwa kwenda Dar tulifurahi sana

na kujiona tulikuwa na bahati

kuchaguliwa kwenda Dar kwani wenzetu

wengi

walikuwa wakililia kupangiwa kazi katika

jiji

hilo.

Kituo changu cha kazi cha kwanza jijini

Dar, kilikuwa kituo cha polisi cha Ilala. Pale

nilipelekwa peke yangu. Wenzangu

walitawanywa katika vituo vingine

vilivyotapakaa sehemu mbalimbali za jiji.

Katika kipindi cha miaka minne ya

mwanzo nilifanya kazi kwa bidii na uaminifu

mkubwa. Kwa vile kazi yenyewe

niliipenda

niliifanya kwa kujituma na kwa weledi.

Mara

kadhaa nilisifiwa na wakuu wangu na

kutolewa mfano kwa wengine.

Siku moja mimi na polisi mwenzangu

tulitakiwa kusindikiza gari lililochukua

mishahara ya wafanyakazi wa kiwanda

cha

bia kutoka benki moja iliyokuwa barabara

ya Samora na kuipeleka kiwandani hapo.

Ilikuwa ni kawaida kila ifikapo mwisho wa

mwezi, mashirika ya serikali huomba

askari

kwa ajili ya kusindikiza mishahara ya

wafanyakazi kutoka benki. Ilikuwa ni nafasi

nzuri ambayo polisi

wadowadogo tulikuwa tunaigombania

kwa

sababu ilikuwa na posho kidogo. Siku

hiyo

nikapata bahati hiyo mimi na mwenzangu.

Tulipakiwa na gari ya kiwanda hicho

lililotufuata kituoni. Mimi na mwenzangu

kila

mmoja alikuwa na bunduki yake aina ya

SMG iliyokuwa na risasi tisini.

Tulipofika benki tulisubiri nje ya gari.

Sanduku la pesa lilipotolewa tulishika

bunduki zetu vizuri na kuangaza macho

kila

upande kuhakikisha usalama wa pesa hizo.

Sanduku hilo lilipopakiwa kwenye gari na

sisi tulijipakia. Gari likaondoka. Tulifika

kiwandani salama. Gari likasimama

kusubiri

kufunguliwa geti ili tuingie ndani ya eneo la

kiwanda.

Wakati askari anakwenda kutufungulia

geti,

gari moja likasimama ghafla ubavuni

mwa gari tulilokuwemo. Ndani ya gari hilo

mlikuwa na watu watano akiwemo

dereva.

Mara tu baada ya gari hilo kusimama

watu

wawili miongoni mwa watano

waliokuwemo ndani, walipenyeza mitutu

ya

bunduki kwenye madirisha na kuanza

kutushambulia kwa risasi za mfululizo.

Mimi na polisi mwenzangu tuliinama

chini. Risasi zilivunja vioo vya gari vya

ubavuni,

zikawa zinapita juu ya vichwa vyetu.

Maafisa

watatu wa kiwanda hicho waliokuwemo

ndani ya hilo gari walipoona

tunashambuliwa walifungua mlango wa

gari wa upande wa pili na kukimbia.

Baada ya maafisa hao kukimbia na

kuliacha

sanduku la pesa ndani ya gari, tulisikia

kimya halafu tukasikia hatua za watu

wakija mbio. Nikahisi walikuwa ni

majambazi

waliokuwa wakitushambulia , sasa

wanalifuata lile sanduku la pesa baada

ya

wenyewe kukimbia.

Hapo hapo nikatoa mdomo wa bunduki

kwenye dirisha na kuanza kufyatua risasi

mwenyewe nikiwa nimeinama.

Mwenzangu

naye alifyatua risasi lakini alikuwa

ameinua

kichwa chake, akapigwa risasi ya kichwa na

kufa pale pale.

Nilipomuona mwenzangu ameuawa

niliacha

kufyatua risasi nikatulia kimya. Nilikuwa

nimeinama chini ya dirisha ili watu hao

wasinione.

Majambazi hao walipoona hatujibu

mapigo

walijua kuwa wameshatuua. Tamaa ya

pesa

ikawafanya waharakishe kufungua mlango

wa gari wakiamini kuwa wameshazipata

pesa hizo.

Vile wanafungua tu mlango huo

walikutana

na mtutu wa bunduki. Niliwafyatulia risasi

majambazi wawili bila wao kutegemea

wakaanguka kando ya mlango wa gari.

Majambazi wengine wawili waliokuwa

nyuma yao walipoona wenzao

wameshambuliwa na risasi zilikuwa

zinaendelea kurindima waligeuka nyuma ili

wakimbie lakini hawakulifikia hata gari

lao

nikawalaza chini wote.

Jambazi mmoja aliyekuwa amebaki

kwenye gari kwenye siti ya dereva aliliondoa

gari

hilo kwa kasi kusalimisha maisha yake.

Sikutakakumkosa yule jambazi,

nikapituka

kwenye siti ya dereva amabayo ilikuwa

tupu. Gari hilo lilikuwa kwenye moto, nikatia

gea

na kulifukuza lile gari.

Wakati naliondoa gari hilo niliwakanyaga

majambazi wawili waliokuwa wamelala

chini na kuwatoa matumbo! Gari hilo

halikufika mbali nikaliingia

ubavuni.

Nililibana na kulibamiza

pembeni mwa barabara kisha nikalichota

na

kulipindua kichwa chini miguu juu, likawa

kama mende aliyekufa huku tairi zake

zikiendelea kuzunguka zenyewe.

Kulikuwa na gari la polisi lililokuwa

kwenye

doria. Polisi hao walipoona tukio hilo

walisimamisha gari. 




Na mimi nikashukuru

kwa kuona nimepata msaada. Nilishuka

kwenye gari nikaona gari jingine la

kiwanda

cha bia likisimama nyuma ya gari la

polisi.

Bila shaka gari hilo lilikuwa likitufuata

nyuma.

Polisi wanne walishuka kutoka gari la

polisi

na maafisa wanne walishuka kutoka gari

la

kiwanda cha bia, watatu walikuwa ni wale

tuliokwenda nao bemki. Nilijua kwamba

walikuwa wakifuatilia pesa zao.

Nikafungua

mlango wa gari nikalitoa lile sanduku la

pesa na kuwakabidhi. 


Itaendelea tena kesho....

Ili usipitwe na simulizi hii kali Hakikisha unaenda sehemu ya followers  una follow hii blog ✨

Post a Comment

0 Comments