Ticker

10/recent/ticker-posts

Mhandisi Victor Seff akagua Barabara Kijiji cha Msomera Handeni Mkoani Tanga,Alipongeza JWTZ

 

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor H. Seff ametembelea miundombinu ya barabara za Kijiji cha Msomera ambapo ni moja ya eneo maalumu lililotengwa na Serikali kwa ajili ya kuwahamishia wafugaji waliokuwa wakiishi katika hifadhi ya Ngorongoro. 

Msimamizi wa Ujenzi wa Mradi wa Makazi ya Wafugaji Kanali S.E Mihayo amempongeza Mhandisi Seff kwa ushirikiano mkubwa unaotolewa na watendaji wa TARURA na akimpongeza Meneja wa Wilaya ya Handeni Mhandisi Eng. Judica Makyao kwa kujitoa kikamilifu kuhakikisha barabara zinafunguliwa na kupitika katika eneo la mradi.

Kanali Mihayo alimueleza Mhandisi Seff eneo la Mradi linahusisha Halmashauri tatu (3) za Wilaya za Handeni, Kilindi na Simanjiro. Alieleza kuwa, utekelezaji rasmi wa ujenzi wa nyumba za Makazi umeanzia katika eneo la Msomera, Wilaya ya Handeni na kwa sasa takribani barabara zote muhimu zimefunguliwa na TARURA.  Kanali Mihayo alimuambia Mhandisi Seff kuwa, awamu ya pili ya ujenzi wa nyumba utafanyika katika Wilaya ya Kilindi na Simanjirio. Kanali Mihayo alieleza kuwa kwa sasa wataamu wa kupanga matumizi ya ardhi “Surveyor” wanaendelea na zoezi la kuzitambua barabara katika eneo la Kilindi na Simanjiro ili ziweze kufunguliwa na kuendelea na ujenzi.

 Meneja wa TARURA wa Wilaya ya Hendeni Mhandisi Judica Makyao alimuambia Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor Seff kuwa, mtandao wa barabara katika Kijiji cha Msomera unajumla ya kilometa 986, ambapo jumla ya kilometa 186 za barabara zimekamilika kuchongwa na kilometa 24 zimewekewa kifusi na changarawe. Alieza kuwa Mkandarasi yupo eneo la kazi na kuendelea na ufunguzi wa barabara pamoja na ujenzi wa Makalavati 10 katika Kijiji cha Msomera

Mhandisi Seff alimpongeza Kanali Mihayo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya Ujenzi wa Makazi ya Wafugaji na kumuahidi TARURA itaendelea kutoa ushirikiano mkubwa na kuhakikisha ujenzi wa barabara unakuwa wa viwango vilivyokusudiwa ili  kufikia adhima ya malengo mazuri ya Serikali inayoongozwa na Mhe.  Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Post a Comment

0 Comments