Ticker

10/recent/ticker-posts

RC Senyamule apokea Pongezi za Spika Tulia Ackson kwa Kuchaguliwa Rais IPU

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule leo Novemba 17,2023 kwa niaba ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson amepokea pongezi za kuchaguliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge DunianI (IPU) kutoka Bw.Ekuzi Elias (Mzalendo Halisi).

Bw. Ekuzi amefikisha pongezi zake kwa kutembea kwa miguu kwa takribani siku tano kutoka Mkoa wa Morogoro hadi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma huku akiwa na bango lililoandikwa ujumbe wa kutoa pongezi kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Dkt. Tulia Ackson.



Dkt. Tulia Ackson alichaguliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani Octoba 27/2023 huku akiwa ni Rais wa 31 na mwanamke pekee kuwahi kuchaguliwa Barani Afrika.

Post a Comment

0 Comments