Ticker

10/recent/ticker-posts

“Wema ni Zaidi Ya Dada Kwangu, Nampenda Sana” Diamond Platnumz


Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini na CEO wa WCB Diamond Platnumz amevunja ukimya juu ya sakata la picha chafu za Msanii wa Bongo movie Wema Sepetu.

Mwezi uliopita Staa Wema Sepetu alipatwa na Janga la mwaka Baada ya kuvujisha picha zake za utupu kwenye mitandao ya kijamii na kuishia kuburuzwa Mahakamani ambako kesi yake inaendelea kuunguruma.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Dizzim Online, Kwa Mara ya kwanza Diamond amefunguka kuhusu sakata hilo la Wema na kuweka wazi kuwa anamheshimu na kuwa alifanya makosa Kama binadamu yoyote.


Wema ni zaidi ya Dada yangu namheshimu na kumpenda sana tulipotokaga Mimi na Wema ni mbali sana na hata Kama hatuna mahusiano lakini urafiki wetu upo na ninaami kila mwanadamu kuna vitu vinatokea ambavyo hatukupangaa vitokee kwaiyo inawezekana walikuwa wamekaa sehemu na hawakupenda vitokee lakini kwa bahati mbaya ikawa hivyo”.


Lakini pia Diamond amemshauri Wema kuwa makini na mambo Kama hayo yasijeyakatokea tena kwani kwa kufanya hivyo atakuwa anawaangusha mashabiki zake wanaompenda Lakini pia anaiangusha serikali inayomtegemea yeye kuwa kioo cha jamii.