Ticker

10/recent/ticker-posts

MAPENZI…FAHAMU MAMBO YA KUFANYA MWANAUME UNAPOKUWA NA MPENZI MWENYE HAMU YA KUJAMIANA KUKUZIDI…..

Baadhi ya wanawake huwa na hamu ya kufanya mapenzi zaidi kuliko wapenzi wao wa kiume. Na wakati mwingine wanaume huwa katika wakati mgumu sana pale wanapokuwa katika mahusiano ama wanapooa wanawake wenye hamu kubwa ya kufanya mapenzi kuliko wao.
Wakati mwingine jambo hili linaweza kuwa la furaha kwani wewe na mwenza wako mnakuwa na wakati mzuri wa kujuana vyema, kutambua anachokipendelea mwenzako katika mapenzi bila kuwa na kikwazo. Lakini kuna wakati jambo hili huweza kuleta matatizo katika mahusiano yenu.
Wanachotakiwa kufanya wanaume ili kuhakikisha wanawaridhisha wapenzi wao wenye hamu ya kufanya mapenzi kuliko wao ili kuhakikisha wanadumisha upenzo na kuepuka masuala ya michepuko.
Msaidie kupiga punyeto
Baadhi ya watu hulichukulia jambo hili kama jambo baya na la aibu. Lakini kiukweli siyo kama wengi wanavyodhani. Unapomsaidia mpenzi wako kupiga punyeto utamsaidia yeye kupata raha na kufikia mshindo na hatimaye ataridhika kuliko kumuacha na ashi, jambo ambalo linaweza kumpelekea yeye awaze kuwatafuta wanaume wengine ili wamridhishe.
Mpe maandalizi mazuri ‘Foreplay’
Kiukweli kabla ya kufanya mapenzi na mwenza wako, inabidi uhakikishe kuwa unamuaandaa vizuri kisaikolojia na kihisia ili muweze kufurahia tendon a mpate kuridhika kwa pamoja. Kuna baadhi ya wanawake huweza kufikia mshindo hata kabla hawajaingiliwa bado. Jaribu kutumia vitu mbalimbali, kumshika maeneo mbalimbali ya mwili wake pamoja na kumuambia maneno matamu ili aweze kuwa tayari kwa kujamiiana. Kufanya hivi kutapelekea wote kufikia mshindo na kuridhika.
Hakikisha hufikii mshindo kabla yake
Kwa mwanaume aliye na mpenzi mwenye hamu kubwa ya kufanya mapenzi, unatakiwa kuhakikisha kuwa mnapokuwa mnajamiiana hufiki kileleni kabla ya mwenza wako. Hii ni kwa lengo la kuhakikisha mwenzako anafurahia mpaka kufikia kileleni.
Kwa kawaida mwanaume anapofika kileleni uume husinyaa na hautokuwa na nguvu ya kutosha kuendelea kudumu ndani ya uke. Hivyo ili uume ubaki kuwa imara, hakikisha unajizuia kufika kileleni mapema mpaka pale mpenzi wako atakapokuwa anakaribia kabisa.
Boresha muda wako wa kurudia tendo ‘Recovery time’
Kuna wanaume ambao baada ya kujamiiana kwa mara ya kwanza, huchukua muda was aa moja mpaka mbili ndipo waweze kuwa tayari kurudia kwa mara nyingine. Kama mwenza wako ana hamu kubwa ya ujamiiana, muda huu kwake utakuwa ni mwingi mno na mwisho wa siku atakereka na hatimaye anaweza kuanza kuwaza kutafuta wanaume wengine ambao watakuwa na uwezo wa kuwaridhisha. Hivyo ili kuepukana na hali hii inabidi ujitahidi kula vyakula ambavyo vitakuongezea nguvu na hamu ya kufanya mapenzi.
Vyakula na matunda kama tikiti maji, tangawizi, samaki wa maji baridi, zabibu, mbogamboga pamoja na chokleti vimetajwa kuwa miongoni mwa vitu vinavyoweza kumuongezea mwanaume hamu ya kufanya mapenzi.