Ticker

10/recent/ticker-posts

KUMBE P SQUARE HAWAJAINGIA KANISANI KUSALI TOKA MWAKA 2007? KISA NI HIKI HAPA…

P Square

Mastaa na maisha yao nyuma ya pazia, mengine ni haya nimeyajua leo toka kwa wakali wa Nigeria, Peter na Paul watoto wa Marehemu Chief Moses Okoye… wamesema toka mwaka 2007  hawaendi kanisani, kisa unajua ni nini?

Jamaa hao ambao kwa pamoja dunia inawajua kama P Square wameingia kwenye Headlines baada ya kufanyiwa Interview na kuyafunua mengine kwamba hawajaenda Kanisani toka mwaka 2007 kwa vile ilikuwa wakiingia tu macho ya watu wote yanakuwa kwao!!
Kila mara tukiingia Kanisani macho ya watu wote yanakuwa kwetu,  wanaacha kumsikiliza Mchungaji.. wanaacha kusali wanaanza kutushangaa“>>> P Square.
p-square3
Tuliona sio vizuri.. ni kama tulikuwa tunasababisha watu waache kufanya kilichowapeleka Kanisani, tukaamua tuache kabisa kwenda Kanisani… Watu wote ni sawa mbele za Mwenyezi MUNGU, sio kitu kizuri watu wakasahau kusali kwa sababu yetu”—P Square.