Kazi ipo! Mwandani wa
staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah
Hassan ‘Zari’ juzikati alizua kizaazaa kisa ujauzito alipohudhuria
kwenye msiba wa aliyekuwa bosi wa Tip Top Connection, Abdul Taletale
‘Abdul Bonge’ aliyefariki dunia ghafla wikiendi iliyopita.
Mwandani wa staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari akiwa kafichwa na bodigadi wake.
Tukio hilo la Zari
lilichukua nafasi katika Kijiji cha Mkuyuni, Tarafa ya Matombo mkoani
hapa ambapo mastaa kibao walisafiri kutoka Dar kwa ajili ya mazishi ya
kiongozi huyo.
ILIKUWAJE?
Awali, katika tukio hilo
lililoshuhudiwa na Ijumaa mapema Jumanne wiki hii, Zari na Diamond,
wakiwa wameongozana na wapambe wao walifika eneo la msiba ambapo kwa
taratibu za Kiislam, wanawake hawachanganyiki na wanaume hivyo Zari
akachukuliwa kwenda upande mwingine huku Diamond akielekea upande wa
wanaume.
HALI YA HEWA YABADILIKA
Akiingizwa garini.
ZARI AIBUA KIZAAZAA
Akiwa upande wa wanawake
wenzake, Zari alijikuta akizungukwa na baadhi ya watu walionekana wazi
kumchunguza kuanzia miguuni hadi kichwani ikidaiwa kuwa, walikuwa
wakicheki kama kweli ana mimba ya Diamond.
“Mwee, huyu ndiye Zari
wa Diamond! Hivi mimba anayo kweli au ndiyo haya mambo ya mastaa wetu,
mhh lakini kweli kitumbo kama kimetuna vile,” alisikika akisema mmoja wa
wanawake hao.Uwepo wa mwanadada huyo uliwafanya wengi kusahau ishu ya
msiba na kujikuta wakipigana vikumbo kumshangaa Zari ambaye muda mwingi
alikuwa akijificha.
Kutokana na mazingira ya
watu kukanyagana kutaka kumuona staa huyo, mrembo aliyefahamika kwa
jina la Jestina George aligeuka kuwa bodigadi wake ili kumuepushia
usumbufu ambapo alifanya kazi ya kumlinda.
PAPARAZI AZUIWA KUMPIGA PICHA
Paparazi wetu aliyekuwa
eneo la msiba kwa lengo la kupata picha za kumbukumbu kwamba Zari
aliwahi kufika eneo hilo, alikumbana na wakati mgumu baada ya Jestina
kumpiga mkwara asijaribu kupiga picha.
Diamond akiimalisha usalama kwa mpenzi wake.
WATU WAANZA ZOGO
Kufuatia kitendo cha
Jestina kumzuia mwandishi wetu kupiga picha, zogo lilianza eneo hilo
huku baadhi ya watu wakihoji sababu za Zari kufichwa.“Au ni hiyo mimba
yake ndiyo maana hamtaki apigwe picha? Acheni hizo bwana,” alisikika
akiwaka kijana mmoja.
PAPARAZI AMFUATA DIAMOND
Baada ya paparazi
kupigwa mkwara asipige picha alilazimika kwenda kumtafuta Diamond ili
ampe ruhusa ya kwenda kumfotoa Zari lakini staa huyo naye alikataa na
kueleza kuwa, kama anataka kufanya hivyo akachukue ruhusa kutoka kwa
meneja wake.
Meneje huyo wa Diamond
aliyefahamika kwa jina moja la Salam alipofuatwa alimruhusu paparazi
kufanya kazi yake lakini aliporudi nyumbani palipokuwa na msiba kwa nia
ya kumfotoa Zari, hali ilikuwa ileile hivyo kumsubiria mpaka Diamond
alipotoka makaburini na alipofika kwenye gari lao, Zari alitolewa kwa
kufichwa na Jestina kiasi cha kuwepo ugumu kupata sura yake.
ZARI AINGIA KWENYE GARI FASTA
Huku watu wakimfuata kwa
nyuma, Jestina alimchukua Zari na kumficha kwapani kisha kumkimbizia
kwenye gari tayari kwa kuondoka eneo hilo.
DIAMOND NAYE APATA WAKATI MGUMU
Wakati Diamond akirejea
kutoka makaburini, alijikuta akizingirwa na baadhi ya vijana ambao wengi
wao hawajawahi kumuona ‘live’ hivyo kumpa wakati mgumu.Hata hivyo, ili
kuwafurahisha, vijana hao walipata fursa ya kupiga naye stori mbili-tatu
kabla ya kuondoka eneo hilo na kuacha umati ukiwasindikiza kwa macho.