Staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Stori: Imelda Mtema STAA wa
sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa, mawigi
wanayovaa mastaa mbalimbali akiwemo yeye, yanawazeesha sura na
kuonekana wakubwa kupita kiasi kumbe sivyo ilivyo.
Lulu alisema, mara nyingi mastaa wanapenda kujaza mawigi makubwa
kichwani mwao lakini kiukweli wakiondoa mawingi hayo na kusuka hata tano
kichwa wataonekana wadogo sana hivyo ni vyema wakabadilika.
“Nilijaribu kuweka mawigi pembeni na kujisukia tano kichwa changu kwa
kweli naonekana katoto kabisa hapo ndipo nilipogundua kuwa mawigi kwa
kipindi kingine siyo kabisa yanatuzeesha tu,” alisema Lulu.