Mahaba
nimalize! Mastaa wapendanao, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul
‘Diamond Platnumz’ wamesababisha tukio jipya kama kawaida yao, safari
hii wameishtua kadamnasi kwa kuzindua gari jipya kwa mahaba mazito ndani
yake, Ijumaa Wikienda lilinyaka mchongo mzima.
Tukio hilo lililojiri kama muvi ya mapenzi (romantic movie) lilitokea
mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Ukumbi wa Golden Jubilee uliopo
Posta jijini Dar wakati Diamond alipokuwa akisherehekea siku yake ya
kuzaliwa na kujizawadia ndinga aina ya BMW X6 ambalo waliligeuza kuwa
uwanja wa malovee wakati walipokwenda kukabidhiwa na menejimenti yake ya
Wasafi.
Awali, waalikwa sambamba na mastaa mbalimbali wakusanyika kwenye
ukumbi huo na ilipofika saa 5:00 usiku, Diamond akiwa ameambatana na
ubavu wake, Wema sambamba na mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’,
waliingia na sherehe kuanza.
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wakila 'romansi'
Baada ya sherehe hiyo kupambwa na matukio mbalimbali zikiwemo bendi
za asili na wasanii, ulifika wakati wa zawadi ndipo wageni waalikwa
walipoanza kujinadi kupitia kipaza sauti na mwishoni ikawa ni zamu ya
menejimenti ya Wasafi ambayo ilitamka kuwa inatoa gari hilo.
0 Comments