Ticker

10/recent/ticker-posts

KAMA MUVI KALI YA MALOVEE...WEMA, DIAMOND WAZINDUA GARI KWA MAHABA..NI BALAA

Mahaba nimalize! Mastaa wapendanao, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wamesababisha tukio jipya kama kawaida yao, safari hii wameishtua kadamnasi kwa kuzindua gari jipya kwa mahaba mazito ndani yake, Ijumaa Wikienda lilinyaka mchongo mzima.
Tukio hilo lililojiri kama muvi ya mapenzi (romantic movie) lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Ukumbi wa Golden Jubilee uliopo Posta jijini Dar wakati Diamond alipokuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa na kujizawadia ndinga aina ya BMW X6 ambalo waliligeuza kuwa uwanja wa malovee wakati walipokwenda kukabidhiwa na menejimenti yake ya Wasafi. 
Awali, waalikwa sambamba na mastaa mbalimbali wakusanyika kwenye ukumbi huo na ilipofika saa 5:00 usiku, Diamond akiwa ameambatana na ubavu wake, Wema sambamba na mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’, waliingia na sherehe kuanza.
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wakila 'romansi' 
Baada ya sherehe hiyo kupambwa na matukio mbalimbali zikiwemo bendi za asili na wasanii, ulifika wakati wa zawadi ndipo wageni waalikwa walipoanza kujinadi kupitia kipaza sauti na mwishoni ikawa ni zamu ya menejimenti ya Wasafi ambayo ilitamka kuwa inatoa gari hilo. 

Post a Comment

0 Comments