Ticker

10/recent/ticker-posts

Mvua Kubwa Kunyesha Kwa Siku Tano TMA Yatoa Tahadhari

Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA), imetoa tahadhari ya uwepo mvua kubwa kwa muda wa siku tano kwenye maeneo machache ya mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia pamoja na Visiwa vya Pemba na Unguja kuanzia Novemba 21-25, 2023.


TMA imetoa angalizo kwa Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari, ambapo athari zinazoweza kujitokeza ni Mafuriko kuathiri maeneo machache, athari kwa usafirishaji, baadhi ya barabara kutopitika na vifo vinaweza kujitokeza kutokana na mafuriko pamoja na kuathirika kwa baadhi ya Shughuli za Kiuchumi.