Ticker

10/recent/ticker-posts

Makamu wa Rais Mstaafu ataka ulinzi kwa Mtoto wa Kiume,ataja Sababu ni hizi hapa

 

Na Sophia Kingimali

MAKAMU wa Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Phumzile Mlambo Ngeuka amewataka wanaharakati wa kifeminia nchini kujikita katika kuelimisha kuhusu ulinzi wa mtoto wa kiume kwa mustakabali wa haki na usawa wa jinsia huku akitoa rai kwa wazazi kuanza kukomesha mfumo dume kuanzia ngazi ya familia.

Amesema ipo haja ya kuwa na majukwaa ya wanaume nchini yenye kueleza yanayowahusu lakini pia kujikita na kuchukua hatua za kupinga ukatili wa kijinsia, wanaopinga ubaguzi dhidi ya wanawake na wanaokataa ndoa za utotoni.

Phumzile amesema hayo novemba 7,2023 jijini Dar es Salaam katika tamasha la 15 la jinsia pamoja na kuadhimisha miaka 30 ya kifeminia la Mtandao wa jinsia nchini (TGNP).

Post a Comment

0 Comments