Ticker

10/recent/ticker-posts

MPYAA: Elimu ya Msingi Sasa Tanzania Kuishia Darasa la Sita, Hii Kuwahusu Walioko Darasa la Tatu Mwaka huu


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Mitaala mipya ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Ualimu itaanza kutumika baada ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023 kupitishwa na Mamlaka za maamuzi ambapo rasimu iliyopo inapendekeza Watoto waliopo darasa la tatu mwaka huu wasome mpaka darasa la sita kisha waende Sekondari, badala ya kuishia darasa la saba.


Prof. Mkenda amesema hayo Jijini Dodoma ambapo amesema tarehe rasmi ya kuanza kutumika kwa mitaala hiyo itatangazwa baada ya kupitishwa kwa Sera hiyo na kwamba itakapopitishwa utekelezaji utaanza kwa awamu.

Mkenda amesema rasimu hiyo inapendekeza Watoto waliopo darasa la tatu Mwaka huu 2023 ndio watakaosoma mpaka darasa la sita, hivyo wale waliopo darasa la nne, tano na sita wataendelea kusoma mpaka darasa la saba.

"Hatima ya yote utekelezaji huu unategemea Mamlaka ya Nchi itakaposema tuanze, matumaini yetu ni makubwa kwamba rasimu hii itapita na siku ya kutangazwa kuanza kwa utekelezaji itakuwa ni siku kubwa katika kuelekea mageuzi ya elimu nchini"

Post a Comment

0 Comments