Ticker

10/recent/ticker-posts

Msanii Harmonize Amkingia Kifua Diamond Platnum Sakata la Kukopi Wanigeria

 

Mwimbaji @harmonize_tz ni kama amemkingia kifua @diamondplatnumz kutokana na shutma zilizozuka za ku-copy baadhi ya nyimbo za wasanii wa Nigeria na vita ya kimuziki inayoendelea kwa sasa kwenye game ya Bongo.

Barua ya wazi ya Harmonize inasema, "Sina chochote cha ku-prove ndani ya nchi yangu, sina hizo nguvu za kupigana na ndugu zangu wa damu".

Teacher Konde akaendelea kusisitiza muungano baina yao kwani ana amini kunaweza fanyika kitu kikubwa zaidi.

"Tujifunze kwa majirani zetu Wanigeria. Mambo ya kuvunjana Moyo kuchambana, kuchekana huyu kakosea huyu hajapatia, tunaoneshana mapungufu na kujishusha wenyewe".

Usiku wa kuamkia leo baadhi ya pages maarufu nchini Nigeria zimefichua ngoma kadhaa ambazo msanii huyo wa Bongo Fleva anadaiwa kuzi-copy. Kitendo kilichopokea ukosoaji mkubwa kutoka kwa wasanii na baadhi ya wadau wa muziki nchini.

Post a Comment

0 Comments