KUHUSU KUOTA UMERUDI UTOTONI AU SHULENI UNASOMA WAKATI SHULE ULISHA MALIZA ZAMANI.
Hii ni ndoto ambayo imekuwa maarufu sana katika siku za hivi karibuni. Siku hizi karibu kila mtu mzima anaota ndoto hii. Sio mara moja wala sio mara mbili ni mara nyingi nyingi.
Wapo wanao ota ndoto hii walau mara moja au mbili kila mwezi, wengine huota mara moja kila wiki na wengine huota karibu kila siku. Wakati mwingine mtu anaweza kuota ndoto hii Zaidi ya mara moja ndani ya usiku mmoja na hali hiyo inaweza kujirudia mfululizo, yani mtu amelala tuseme saa nne usiku , saa sita usiku anaota ndoto hiyo, anastuka. Akilala tena anaiota ndoto hiyo hiyo.
NINI MAANA YA NDOTO HIZI MBILI ; KUOTA UPO SHULENI UNASOMA AU UPO UTOTONI NA KUOTA UPO SHULE UNAFANYA MTIHANI AMBAO ULISHA UFANYAGA MIONGO KADHAA ILIYOPITA AU MIAKA MINGI ILIYOPITA ?
Tuanze na ndoto ya kuota UPO SHULENI UNASOMA WAKATI WEWE ULISHAMALIZAGA SHULE MIAKA MINGI SANA IMEPITA.
Ulimaliza darasa la saba mwaka 1994 na kuendelea na masomo ya juu. Sasa hivi umeshakuwa mtu mzima mwenye watoto na pengine wajukuu kabisa. Lakini unalala usiku unaota ndoto umerudi shuleni katika darasa hilo hilo la saba au hata chini ya hapo. Upo katika mazingira ya shule ulio kuwa unaisoma. Katika ndoto yako hiyo mazingira ya shule yako huwa ni yale yale yaliyo kuwepo kipindi unasoma hata kama katika ulimwengu wa nyama yameshabadilishwa. Mfano kulikuwaga na miti mikubwa labda sasa hivi imeshakatwa. Kulikuwa na sehemu ya wazi na sasa hivi imejengwa madarasa mengine. Wewe katika ndoto yako utakuwa katika mazingira yale yale yaliyo kuwepo mwaka huo wa 94 wakati bado unasoma katika shule hiyo.
JE NDOTO HII INA MAANA GANI ?
Dhana iliyo jengeka miongoni mwa watu wengi katika jamii ni kwamba ukiota ndoto hii basi maana yake ni...