Rais Mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta, akila kiapo mbele ya Jaji Mkuu, DavidMaranga |
Nairobi
Rais wa leo Novemba 28, 2017 ameapishwa leo kwenye sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Kasarani, Jijini Nairobi, Kutoa hotuba nzito na yenye kujaa matumaini.
Katika hotuba yake iliochukua takribani dakika 45, na kurushwa mubashara(live) na vyombo mbali mbali vyo redio runinga na mitandao ya kijamii ya Tanzania na Kenya mashirika ya habari ya kimataifa. amesema kuwa atadumisha upendo na amani kwa wakenya.
Aidha amesemakuwa kuwa kamwe hawezi kujenga chuki kwa raia ambao hawakumchagua.
Rais Kenyatta ameongeza kuwa anati kushrikiana na kwa Wakenya wote na kuwa siasa zimeisha ninachobaki ni kushirikiana na kuwa shauku alionao kwa sasa ni kuwaletea Wakenya maendeleo na si vingnevyo.
Rais huyo wa taifa ya Kenya lenye uchumi mkubwa Afrika Mashshariki amesisitiza kuwak yeye na wakenya tunajua kuwa kenye ndio nyumbani
“ Ndugu zangu zangu Wakenya hapa mimi na nyie hapa ndio nyumbani na hakuna pahala pengine.” Amesema Rais Kenyetta.
Katika hatua nyingine Rais Kenyatta ameahidi kuwa ataongoza kwa Jamhuri ya Kenya kwa utawala wa sheria na kulinda katiba ya nch hiyo
“Nitaitetea na kuilinda katiba ya Kenya”.
Vilevile ameahidi kuwa hatabagua mtu kwa misingi ya dini, ukabila, utamaduni au makundi yeyote ya jamii yoyote ya Wakenya
“Wakaka na wadada naahidi kuwa sitobagua mkenya yeyote kwa misingi ya ukabila, rangi au kundi Fulani ndani ya Kenya” Amesisitiza
Sherehe hizo zimehudhuriwa na Mrais na vingozi mbali mbali wa Afrika na Nje ya Afrika, Tanzania imewakilishwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.