Ticker

10/recent/ticker-posts

EXCLUSIVE : KAJALA MASANJA AAMUA KUMRUDIA MUNGU,AOKOKA AFUNGUKA SIRI NZITO


EXCLUSIVE!! Kwa mara ya kwanza, mrembo kunako filamu za Kibongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa ameokoka hivyo ameamua kumrudia Mungu kwa sababu anaona mambo ya kidunia kwa wakati huu hayana nafasi na si ya kuyaendekeza.

Akizungumza   Kajala alisema kwa sasa ameamua kuabudu kwenye kanisa moja la kiroho lililopo Kibamba jijini Dar na kukiri kuwa tangu ajiunge huko, amekuwa akifunguliwa mambo yake mengi ikiwa ni pamoja na kujitambua.
“Nimeamua kwa akili yangu mwenyewe kurudi kwa Muumba wangu kwa sababu haya mambo ya kidunia yana mwisho wake na hata mastaa wenzangu wanapaswa kumuabudu Mungu hata kwa juma mara moja kwa maana chochote walicho nacho ni kwa ajili ya yeye,” alisema Kajala.