Ticker

10/recent/ticker-posts

LULU AMRITHI ZARI...FAMILIA YA DIAMOND WAANIKA KILA KITU!

Staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’.
Madai mazito! Siku chache baada ya kubainika kuwa uwezekano wa mzazi mwenzake na ‘kichaa’ wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kurudi Bongo na kuendelea na uhusiano na jamaa huyo ni mdogo, hatimaye familia ya staa huyo imemtaja Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ kuwa ndiye mrithi wa Zari, Amani lemeelezwa. Habari kutoka kwa vyanzo tofauti kwa nyakati tofauti vimenyetisha hivi karibuni ana kwa ana na kwa njia ya simu kuwa, kuna vielelezo vilivyoshiba vya kuthibitisha ukaribu wa Lulu na Diamond huku vikibashiri kwa mifano iliyo wazi kuwepo kwa uwezekano wa wawili hao ‘kuunganisha mbavu’ na kuishi kama mke na mume.
Katika maeneo tofauti vyanzo hivyo viliweka wazi kwamba, miongoni mwa sababu zilizofifisha upendo wa Zari kwa Diamond ni pamoja na kushtukia uhusiano usiofaa wa wawili hao.

ZARI AFUMA SMS TAMTAMU
Vyanzo hivyo vilidai kwamba, kabla ya kutimka Bongo, mara kwa mara Zari alifuma vielelezo vingi vilivyoashiria ukaribu wa Lulu na Diamond.Moja ya vielelezo hivyo ni ujumbe mfupi wa maneno (sms) kutoka kwa Lulu kwenda kwa Diamond zilizokuwa na maneno matamtamu ya kimapenzi.

DADA ZAKE DIAMOND WATAJWA
Habari hizo zilidai kwamba, mara kadhaa, kila ulipokuwa ukiibuka ugomvi mkubwa kati ya Diamond na Zari, wifi zake (dada zake Diamond) walikuwa wakiingilia kati kwa kumwaminisha Zari kuwa Lulu ni rafiki wa karibu wa kawaida, jambo ambalo Zari alikuwa akiliafiki kwa shingo upande.“Kwa kweli Lulu ameharibu uhusiano wa Diamond na Zari, unajua ukaribu wake na Diamond unaonekana ulianza zamani sana.



Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’. BETHIDEI YA ROMY JONES
“Lakini sasa umejidhihirisha, hata siku ya sherehe ya kuzaliwa ya Romy Jones (binamu na DJ wa Diamond), Lulu alionekana akijiachia waziwazi na Diamond, jambo lililoibua viulizo. Katika ishu hiyo Lulu alidaiwa kuwa anamchokonoa Zari ambaye aliachwa nyumbani na mtoto (Tiffah) kwani ilikuwa siku chache sana baada ya kujifungua.

BETHIDEI YA DIAMOND
“Kama hiyo haitoshi, kwenye bethidei ya Diamond iliyofanyika kule nyumbani kwa jamaa (Madale-Tegeta jijini Dar), Lulu alitumia muda mwingi sana kuwa karibu na Diamond, hali iliyoibua maswali na minong’ono mingi kwani ilikuwa ni siku chache tu baada ya Zari kutimkia Afrika Kusini,” ilisema sehemu ya taarifa kutoka kwa vyanzo hivyo na kuongeza:“Kinachoonekana, familia ya Diamond imekubali Lulu awe mrithi wa Zari kutokana na ukaribu wake na familia hiyo.”

WAHUSIKA WATAFUTWA
Baada ya kunyetishiwa habari hiyo, kwa kutambua wajibu na weledi wao kikazi, wanahabari wetu waligawana majukumu kwa kuwatafuta wahusika ambao ni Lulu, Diamond na familia ya Diamond ambayo ilionesha kukubali Lulu kuwa mrithi wa Zari.

FAMILIA YA DIAMOND
Mmoja wa waandishi wetu, alizungumza na familia ya Diamond, wakiwemo na dada zake (Esma Platnumz na Queen Darleen) pamoja na wanafamilia wengine ambao hawakuonesha kinyongo juu ya Lulu na kwamba anafaa kuwa mmoja wa wanafamilia hiyo (kwa maana ya kuolewa na Diamond).

NDUGU WA DIAMOND AANIKA
“Yeah, jamani tulishasema, kaka yetu hana mipaka na mtu, kwa Lulu hana kipingamizi na mbona uhusiano wao uko wazi?“Kwanza Lulu ni binti mzuri, ana utulivu na maadili ya kuwa mke wa mtu, hatuna shida naye, akikubaliana na Nasibu (Diamond), sisi tunamkaribisha kwa mikono na miguu yote,” alianika Esma, mmoja wa dada zake na Diamond kwa niaba ya familia.
DIAMOND ABANWA
Ili kukoleza uhondo wa habari hii, mwandishi wetu mwingine alimtafuta Diamond na kumbana vilivyo juu ya ishu hiyo ambaye kwa macho ya ‘kaka mbona unanibana hivyo’ alisema ni heri mambo hayo yaachwe ili kuepusha kile alichokiita ‘…mgogoro usiokuwa wa lazima’.
“Naomba haya mambo myaache kwa familia yangu, wakati mwingine ni busara kuacha mambo fulani yapite kama yalivyo, nimekuwa karibu na Lulu kwa muda mrefu sasa, acha iwe hivyo na mambo hayo yaishe,” alisema Diamond kwa lugha ya kimafumbo huku akimtupia mwandishi wetu jicho la ‘achana na mambo hayo bwana’.
LULU AMSINGIZIA WEMA
Kama tulivyosema, waandishi wetu walijipanga vyema kuhakikisha msomaji wetu unapata kila kitu kuhusu habari hii, tena kwa undani hivyo mwanahabari wetu wa mwisho katika orodha hii alimnasa Lulu kwenye bethidei ya Wema Isaac Sepetu wikiendi iliyopita na kumuuliza kwa udadisi wa kina juu ya madai hayo ambapo kwa sentensi za kiutu uzima alisema:
“Mimi nitoke na Diamond! Naanzaje kwanza? Halafu ningekujaje hapa kwenye shughuli ya Wema wakati jamaa (Diamond) ni ex-girlfriend (mpenzi wa zamani) wa Wema? Hakuna kitu kama hicho. Kwanza ni mtu wangu wa karibu tu.”
TUJIKUMBUSHE
Kabla ya kila mmoja kufunguka, kumekuwa na madai ya muda mrefu kuwa kuna kila dalili wawili hao wakawa pamoja kwani wamekuwa wakifanya mambo yao kwa ushirikiano wa hali ya juu lakini mara nyingi kwa usiri mkubwa.
Imendikwa na Brighton Masalu, Musa Mateja na Imelda Mtema.