MSANII wa maigizo na filamu nchini, Amri
Athumani ‘Mzee Majuto’ ameeleza kuwa, kwa furaha aliyonayo baada ya
kupata safari ya kwenda Uturuki imemfanya ajisikie kufa kwani ni bahati
ambayo hakuitarajia.
Mzee Majuto amepata shavu akiongozana na
wasanii wengine wawili, Vicent Kigosi ‘Ray’ na Steven Jacob ‘JB’ ikiwa
ni mualiko wa Balozi wa Uturuki nchini, Ali Davutoglu na mkewe Yasim kwa
udhamini wa Princes Casino. Akizungumzia safari hiyo, Mzee Majuto
alisema:
“Kwa kweli furaha niliyonayo najisikia
kufakufa tu, ngoja ninyamaze kwa sababu bila hii safari huenda ningedoda
hapa Tanzania mpaka nakufa, nashukuru sana watu wa Princes.”
Mastaa wengine waliotakiwa kuwemo kwenye
msafara huo ni pamoja na Aunt Ezekiel na Wema Sepetu lakini kutokana na
kubanwa na majukumu mengine, wameshindwa kuondoka