ALIYEKUWA mtangazaji
wa kituo cha redio cha Efm, Peniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa
tabia ya baadhi ya wasichana mastaa kujiona masista duu itawamaliza kwa
sababu watajikuta uzee unawakabili bila kuwa na ndoa.
Akizungumza na gazeti hili, Penny alisema mastaa wengi wanapenda kujiona
ni matawi ya juu na kufikia hatua ya kudharau watu wengine kiasi kwamba
hata wenye mapenzi ya dhati kwao hujikuta wakijiweka pembeni hivyo
kuwafanya ‘kuchina’ wakati wakitafuta ndoa.
“Unajua kuna vitabia fulani hivi mastaa tunavyo, ya kisista duu ambayo
inatufanya tuchine, maana wengi si wanatuogopa wakidhani sisi ni matawi
ya juu wakati ni wa kawaida sana,” alisema Penny.