Ticker

10/recent/ticker-posts

HAWA NDIO WAIGIZAJI WA MOVIE WA KIUME MATAJIRI ZAIDI DUNIANI

Fast Seven
Time hii nimeona nigeukie kwenye sekta ya movie mtu wangu, hapa nimekusogezea list ya waigizaji wa movie ambao ndio wamekaa kwenye top 10 ya utajiri mwaka huu 2015 kutoka Industry ya Marekani yaani Hollywood na India (Bollywood).
Icheki hii list hapa, huenda kuna staa wako unaemkubali yuko hapa…
1. Mel Gibson
mel
Utajiri wa staa huyu wa Hollywood ni kama dola Mil. 600 na kwa mwaka anaingiza zaidi ya dola Mil. 72.
2. Shahrukh Khan
shak
Staa wa Bollywood, utajiri wake ni dola Mil. 600 sawa na Mel Gibson.. Anaingiza jumla ya dola Mil. 72 kwa mwaka.
3. Jack Nicholson
jack
Utajiri wa staa huyu ni dola Mil. 400, kipato chake kwa mwaka anaingiza dola Mil. 48.
4. Sylvester Stallone
mojaaa
Wengi wanamfahamu kama ‘Rambo‘, staa wa Movie za action Marekani. Jamaa nae yumo yani, utajiri wake ni kama dola Mil. 400, bado kwa mwaka ana wastani wa kungiza dola Mil. 48 kwa mwaka.
5. Tom Cruise
Knight And Day - UK Film Premiere - Red Carpet Arrivals
Utajiri wake ni dola Mil. 380, bado anakusanya mkwanja wa kutosha yani, kwa mwaka ni kama dola Mil. 46.
6. Johnny Depp
sita
Yuko nafasi ya sita, utajiri wake ni dola Mil. 350.. kwa mwaka bado ana kipato kinachofikia dola Mil. 42.
7. Tom Hanks
tom
Ana utajiri wa dola 350,000,000 na kila mwezi hupokea kiasi cha dola 42,424,242
anold
Mbali na kuwa actor maarufu duniani, aliwahi kuwa Governor wa California kuanzia mwaka 2003 mpaka 2011. Yuko nafasi ya nane, utajiri wake ni kama dola Mil. 300, bado anapiga kazi na anakadiliwa kuingiza kama dola Mil. 36.
9. Michael Douglas
tisa
Jamaa ni kama wanalingana na Arnold hivi, nae ana utajiri wa dola Mil. 300 pamoja na kuingiza dola Mil. 36 kwa mwaka.
10. Adam Sandler
adam
Huyu jamaa ni mmoja ya mastaa wa Hollywood, kaonekana na kwenye Movie ya Grown Ups2 pamoja na mastaa wengine kama Chris Rock. Utajiri wake ni dola Mil. 300, kwa mwaka pia kipato chake ni kama dola Mil. 36, sawa na Michael Douglas.