Siku
chache kupita baada ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (CHADEMA), Mabere Marando kufichua njama za Mlinzi wa
Katibu Mkuu wa Chama hicho Wilbroad Slaa, bwana Khalid Kangezi kupanga
mipango ya kumuua katibu huyo huku akishirikiana na Vigogo wa Chama
Mapinduzi CCM pamoja na Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Kinondoni,naye
Mlinzi huyo ameibuka na kufichua siri nzito ndani ya Chama hicho
kikuu cha upinzani nchini..
Akifichua
siri hiyo leo mchana Jijini Dar es Salaam mbele ya Waandishi wa
habari, Kangezi amesema amesikitishwa sana na madai ya uongo
yanayoenezwa na viongozi wa CHADEMA huku wakificha ukweli wa Mambo
kwani ukweli wa yeye kuzushiwa uongo huo unatokana na kuwa na mahusiano
na Mke wa Dr. Slaa .
“Nawashangaa
sana hawa Viongozi wa Chadema wanaosema mimi ni nimehusika katika
mipango ya kumuua Dr. Slaa. Wanaficha ukweli tu kwani sababu ya
kuzushiwa uongo huu inatokana na mimi kuwa na mahusiano mabaya na Mke
wa Slaa...
"Nilipoenda kumwabia Slaa, alisema niende nikamalizane na mke wake lakini ukweli ni kuwa mambo hayakwenda vizuri, mke wake hakunielewa , ndipo Slaa akapeleka sakata hilo kwenye uongozi wa juu” amesema kagenzi na kuongeza:
"Nilipoenda kumwabia Slaa, alisema niende nikamalizane na mke wake lakini ukweli ni kuwa mambo hayakwenda vizuri, mke wake hakunielewa , ndipo Slaa akapeleka sakata hilo kwenye uongozi wa juu” amesema kagenzi na kuongeza:
"Baada ya Dr. Slaa kupeleka ugomvi huo kwenye ngazi za juu,juzi wakati naenda ofisini nilikamatwa na kupelekwa chumba cha mateso kinacho milikiwa na Chama hicho"
Bwana
Kagenzi ameendeleo kusema kuwa hata madai wanayodai kwamba anauhusiano
wa karibu na usalama wa Taifa pamoja na Vigogo wa CCM ni ya uongo.
“Jamani
hivi inaingia akilini kweli mimi leo na maisha yangu haya niwe na
uhusiano na watu wa usalama na CCM,huu ni uongo wa hali ya juu na
wanataka kunichafua kwa jamii tena niseme ukweli chama hiki kinataka
kuficha ukweli juu ya mambo waliyonitendea.
“Mimi
nimekuwa mlinzi wa Dr. slaa kwa muda wa miaka mingi sana ,tena nilikuwa
nampikia na kumtengea hadi chai ya kunywa eti leo niambiwe naandaa
mipango ya kumuua ? Huo ni unafiki” amesema Kagenzi
Mlinzi
huyo ameenda mbali zaidi na kufichua mipango ya kigaidi
inayofanywa na Chadema huku akisema wameandaa ofisi ya utesaji.
“Chama ambacho kinandoto ya kuchukua nchi leo kinaandaa mipango ya mauaji na utesaji kama walivyonifanyia .
"Waliniteka na kunifungia kwenye chumba cha mateso wanachomiliki wao, wamenichoma visu na kuniweka kwenye Mashine ya umeme bila kosa lolote,eti wakinishinikiza nitaje wanaonituma. Jamani nawaambia ukweli na watanzania wajue, situmwi na mtu yeyote” .
"Waliniteka na kunifungia kwenye chumba cha mateso wanachomiliki wao, wamenichoma visu na kuniweka kwenye Mashine ya umeme bila kosa lolote,eti wakinishinikiza nitaje wanaonituma. Jamani nawaambia ukweli na watanzania wajue, situmwi na mtu yeyote” .
Aidha, Kagenzi amekitupia lawama chama hicho na kusema kuwa mateso waliyomtesa yamemfanya apoteze nguvu za kiume .
Kuhusu
kuingiziwa Milioni saba kwenye simu yake na watu wa Usalama wa Taifa,
Kagenzi amesema hizo ni taarifa za uongo kwani hata simu yake haina
salio na haijawahi kupokea pesa hizo.
Kagenzi
amehitimsha kwa kusema kuwa baada ya mahojiano na jeshi la
polisi sasa anajipanga kufungua kesi mahakamani ili kuwashitaki
CHADEMA kwa mateso waliyompa.