Muigizaji, mtayarishaji na muongozaji wa filamu, Jacob Stephen aka JB anatarajia kuachia filamu mpya wiki ijayo iitwayo Mzee wa Swaga.
Filamu hiyo iliyotayarishwa chini ya kampuni ya Jerusalem Film imeigizwa na wasanii mahiri akiwemo JB, Cassie Kabwita, Wastara, Wellu Sengo, Thea Mike, Ndubagwe Misayo na wengineo.
Kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram aliwahabarisha mashabiki na kuandika hivi; ‘MZEE WA SWAGA ITAKUWA MTAANI WIKI IJAYO’–@jb_jerusalemfilms