Ni
kama vile hakukua na vita ya maneno dhidi ya watu wawili maarufu 50
Cent na bondia Floyd Mayweather baada ya wawili hao kuwasiliana kwa nia
ya mtandao wa kijamii Instagram kuhusiana na tukio lilstaajabisha watu
wengi la Rapper asie maarufu sana Earl Hayes aliemuua mkewe Stephanie
Moseley na kisha kujiua mwenyewe
Katika tukio hilo imeminika kua Floyd
mayweather alishuhudia tukio hilo liliofanynwa na Hayes baada ya
kupigiwa simu nae na kisha kutekeleza mauaji hayo huku akishuhudia kwa
njia ya simu.Hayes alikua akimtuhumu stephanie kua si muaminifu katika
mahusiano yao.
50 cent kupitia mtandao wa Instagram
alimuandikia ujumbe ulionekana akisikitikia tukio hilo la kushtua na pia
kumtaka awe katika hali ya faraja baada ya kuwa katika wakati mgumu kwa
kushuhudia mauaji hayo.
“@floydmayweather you are my little
brother. All can think about is what you said to me up stairs. Don’t you
ever do nothing to your self no matter what champ. We can fall out and
fight or what ever,but I don’t want to see you go out like that.”
ilisomeka sehemu ya ujumbe kutoka kwa 50 cent kwenda kwa bondia huyo
ambapo bondiua huyo alirepost ujumbe huo toka kwa 50 cent kuonesha
kupokea kile ambacho kimeandikwa kuelekea kwake.
Sehemu ya ujumbe imeonesha 50 akimuita
bondia huyo mdogo wake jambo ambalo halikua likionekana kwa muda sasa
kufuatia wawili hao kukorofishana kwa kile kilichoaminika matatizo ya
kibiashara baina yao