Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo
amefikisha mabao 22 na kumfikia mpinzani wake,nyota wa Liverpool Luis Suarez wa Liverpool
katika mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu barani Ulaya.
Ronaldo alifunga bao moja katika
pambano dhidi ya Granada Jumamosi iliyopita katika ushindi wa mabao 2-0
wa Real Madrid na Suarez alikuwa akicheza mechi ya Kombe la FA dhidi ya
Bournemouth.
Mastaa hao wawili wamemwacha kwa
tofauti ya mabao matatu mshambuliaji wa Atletico Madrid, Diego Costa
ambaye bao lake katika ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Rayo Vallecano
lilihesabiwa kama bao la kujifunga kwa Saul Niguez.
Mshambuliaji nyota wa Heerenveen ya
Uholanzi, Alfred Finnbogason amepanda hadi nafasi ya nne baada ya
kufunga bao la 19 la msimu katika kichapo cha mabao 3-1 cha timu yake
dhidi ya Cambuur. Chanzo: www.goal.com
0 Comments