Ticker

10/recent/ticker-posts

RONALDO, SUAREZ SASA NGOMA DROO...

suarez f6f66
Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amefikisha mabao 22 na kumfikia mpinzani wake,nyota wa Liverpool  Luis Suarez wa Liverpool katika mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu barani Ulaya. 


Ronaldo alifunga bao moja katika pambano dhidi ya Granada Jumamosi iliyopita katika ushindi wa mabao 2-0 wa Real Madrid na Suarez alikuwa akicheza mechi ya Kombe la FA dhidi ya Bournemouth.
Mastaa hao wawili wamemwacha kwa tofauti ya mabao matatu mshambuliaji wa Atletico Madrid, Diego Costa ambaye bao lake katika ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Rayo Vallecano lilihesabiwa kama bao la kujifunga kwa Saul Niguez.
Mshambuliaji nyota wa Heerenveen ya Uholanzi, Alfred Finnbogason amepanda hadi nafasi ya nne baada ya kufunga bao la 19 la msimu katika kichapo cha mabao 3-1 cha timu yake dhidi ya Cambuur. Chanzo: www.goal.com

Post a Comment

0 Comments