Ticker

10/recent/ticker-posts

Spika Tulia Ackson: Wanaojitolea wapewe kipaumbele Utumishi

 Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson ameishauri Serikali kuweka utaratibu wa dharura wa kuwapa kipaumbele Wafanyakazi wa kujitolea kwenye suala la ajira wakati mchakato wa sheria ya Wafanyakazi wa kujitolea ukiendelea kuchakatwa.

“Katika kipindi hiki cha kusubiri wakati Serikali mkijipanga maadam wapo, hizo kada mbalimbali za watu wanaojitolea mtafute utaratibu wa muda ama wa mpito wa kuwatazama wakati mnasubiri kufanya marekebisho makubwa kwa sababu wapo na wanaendelea kujitolea.” Ameshauri Spika Tulia

Ameyasema hayo Bungeni jijini Dodoma katika mkutano wa 12 kikao cha tano Septemba 04, 2023 baada ya Mbunge wa Kiteto, Edward Ole Lekaita kumuuliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora ni lini Serikali itapeleka marekebisho ya Sheria ya Ajira ya Utumishi wa Umma kuongeza kigezo cha kujitolea ili kutoa fursa kwa wanaojitolea.

Post a Comment

0 Comments