Ni mazoea ambayo watu wake wamekua nayo kwamba akiwa na tukio kama
hili basi ni lazima atalifanya kwenye mojawapo ya club za usiku Dar es
salaam kama alivyokua akifanya mara nyingi lakini this time staa huyu
anaelipwa ghali zaidi kwenye show zake ambae pia siku zake za kupumzika
mara nyingi ni jumatatu au jumanne ameenda kwenye levo nyingine.
Diamond Platnumz kesho August 29 2013 anategemea kuitambulisha kwa
fans wake video yake mpya kabisa ambayo picha zake zilisambaa kwenye
mtandao ambapo ameishoot Afrika Kusini na hili tukio litafanyika kwenye
hotel ya kifahari Dar es salaam… Serena.
Diamond mwenyewe anasema hakutakuwa na kiingilio kwenye uzinduzi huo lakini wataofika ni wale waliopewa mwaliko
maalum kuingia kwenye hii hoteli maarufu ambayo ilizoeleka pia
kuwahudumia mastaa wakubwa wa muziki kama Fabolous, Koffi Olomide na
wengine lakini this time Diamond Platnums amekodi ukumbi alafu hataki
watu walipe kiingilio, yani anaalika tu.
0 Comments