Ticker

10/recent/ticker-posts

TARURA KUANZA UJENZI WA BARABARA YA KASULU -KABANGA-KASUMO-MUYAMA HADI BUHIGWE KWA KIWANGO CHA LAMI

 


Mwandishi wetu leo amefanya mahojiano na mtendaji mkuu  wa TARURA  na kumweleza kuhusu hatua iliyofikiwa kwa Moja ya Barabara ya Kasulu- Kabanga-Kasumo-Muyama  iliyoko wilayani Buhigwe Mkoani Kigoma  inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha Lami ambapo mkandarasi tayari ameshasaini mkataba wa ujenzi huo unaotarajiwa kuchukua kipindi cha mwaka mmoja.
Akizungumza na mwandishi wetu Mtendaji mkuu wa Tarura Mhandisi Victor Seff amesema kuhusu barabara ya Kasulu Kabanga  tayari kila kitu kimeshakamilika kuanzia michakato ya kumpata kandarasi hadi mkataba wa ujenzi huo umeshasainiwa hivyo mkandarasi anatarajiwa kuanza kazi hiyo wakati wowote kutoka sasa.
...TARURA  tunakuwa na mipango yetu kwa kila mwaka ambapo mwaka huu wa fedha wa 2022/2023 moja ya kazi tuliyopanga kuifanya ni kuhakikisha hii barabara ya Buhigwe inajengwa kwa kiwango cha Lami na yote ina umbali wa kilomita 35 ambapo kwa kuanza tumeanza awamu ya kwanza na kusaini mkataba wa kujenga  Kilomita 12.5 kisha baada ya hapo tutaendelea na kipande kitakachobakia.

Post a Comment

0 Comments