Ticker

10/recent/ticker-posts

RAIS SAMIA SULUHU ATOA MALEKEZO HAYA MAZITO LEO…BEI KUSHUKA YA MAFUTA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ameamzungumza na wananchi leo 09/05/2022 kupitia vyombo mbalimbali vya habari akiwa ikulu jijini Dar es Salaam huku ajenda kuu ikiwa ni kuwaelezea wananchi namna serikali ilivyoamua kuweka mikakati maalum wa kuwasaidia wananchi kutokana na kupanda kwa gharama za maisha kuliko sababishwa na kupanda kwa bei za mafuta katika soko la dunia.

Aidha katika hotuba yake hiyo Rais Samia amemuagiza waziri wa nishati Mhe January Makamba kutoa ufafanuzi bungeni kesho juu ya hatua zitakazochukuliwa na katika kupunguza bei ya mafuta na kuwasaidia wananchi kupunguza ukali wa maisha ambapo Rais Samia amesema gharama hizo zitashuka kuanzia tarehe 01/06/2022.



Post a Comment

0 Comments